Tuesday, February 27, 2018

Andika Mawazo Yako na Ukae Kimya

Watu wengi wana mawazo mazuri, wana ndoto kubwa, lakini mojawapo ya sababu ya kwanini hakuna kinachofanyika ni kwamba wengi tunaongea sana. Utakuta mtu ndo kwanza amepata wazo la kufanya kitu fulani, lakini saa hiyo hiyo anaanza kuwashirikisha anaowaita marafiki zake. Na kuanzia hapo inakuwa kila siku ni...

Friday, February 23, 2018

Thamani ya Maisha Kabla ya Kifungua kinywa ni Ipi?


“Fikra ni viumbe hai” ~ Swami Sivananda
Siku zote, maisha ni kile ufanyacho kuanzia pale unapoamka kitandani asubuhi hadi pale unapokwenda kulala au unapomaliza siku yako. Kwa maneno mengine ni kwamba, kila unapoamka mapema asubuhi, maana yake umeanza maisha upya. Wengi wetu hatujaweza kutambua thamani kubwa iliyopo katika masaa haya ya kuanzia tunapoamka kitandani hadi pale tunapopata kifunguakinywa. Ukweli ni kwamba, masaa ya kabla ya kifunguakinywa ni