Monday, August 28, 2017

Fursa Nyingi Tuko Maskini Kwanini?


Mapema leo 28/08/2017, nilikuwa naangalia na kusikiliza video juu ya kongamano la wadau wa zao la mpunga, lililofanyika kuanzia tarehe 14-18 mwezi septemba 2015. Mkutano huo ulihusisha zaidi wanasayansi na wataalam wa kilimo cha mpunga. 

Katika mkutano huo, mmoja wa washiriki ambaye ni Profesa Nuhu Hatibu aliwasilisha mada yake iliyojulikana kama “Biashara ya kikanda kwa mazao ya chakula kama nyenzo ya kuufanya utafiti utumike katika kutengeneza utajiri” au kwa lugha ya Kingereza; “Regional Trade in Food Staples as an Instrument for Getting Research into use for Wealth Creation”. Katika video hiyo Profesa Nuhu Hatibu, alitoa nasaa za maana sana na akaeleza

Monday, August 14, 2017

Unajua Kwanini Kwanini Yako ni Muhimu?


"Kwanini yako" ndiye mlizi wako dhidi ya changamoto na wakatisha tamaa" ~ Cypridion Mushongi
Kwa mtazamo wa kimafanikio, kuweza kuuishi ukweli ni muhimu katika kufikia malengo yako hasa, uhuru wa kipatao/fedha. Jaribu kufikiria ulipokuwa bado mdogo, wakubwa zako walikuuliza unataka nini ukikua, pengine ulisema unataka kuwa mwanasayansi mashuhuri, mpishi, mwimbaji au daktari wa mifugo n.k. Na unaweza kukumbuka walionekanaje ulipowapa majibu hayo? Yawezekana walikukatisha tamaa kwamba haiwezekani au walikutia moyo kwa kukwambia kuwa unaweza ukawa mtu yeyote unayetaka kuwa, ilimradi

Monday, August 7, 2017

Sababu za Wateja Kuwa Zaidi ya Bosi ni Hizi Hapa


Katika maisha yetu ya kila siku, matendo yetu sikuzote yanadhihirisha na kuthibitisha kile tunachofikiri na kuwaza. Hii ndiyo kusema kwamba, kitu cha kwanza na muhimu kuwa na maisha bora yanayoambatana na uhuru wa kifedha ni jinsi tunavyofikiri na kutenda. Watu wengi wanafikiri mpaka watakapokuwa na mali nyingi ndipo watajiita au kujiona matajiri. Suala la kuwaza wengi wetu hatulipi kipaumbele, kiasi kwamba wengine wanadhani kukaa na kufikiri ni