Saturday, October 31, 2015

Tuesday, October 27, 2015

Fanya Mambo 5 Leo Kufaidi Nguvu ya Fikra Zako

Fanya Mambo 5 Leo Kufaidi Nguvu ya Fikra Zako


Fikra zetu kutoka ndani ya akiri zetu ndiyo kila kitu. Fikra ndilo dirisha unalotumia kuangalia dunia na mambo yake yote. Ukishakuwa umelitabua hili utakubaliana na mimi kuwa unahitaji kuanza mara moja kujitathimini juu ya mwenendo wako. Unahitaji, kujenga na kuinua heshima yako juu na hii ikiwa ni pamoja na kupanua dirisha lako la fikra ili kuona zaidi fursa za mafanikio. 

Ili kupanua dirisha la fikra, inabidi kutunza  kujiamini na kujikinga dhidi ya athari zitokanazo na changamoto mabalimabali za kimaisha. 

Na hapa unahitaji kufahamu mambo 5 yatakayo kuwezesha kufanya uchunguzi wa undani ya fikra zako na hatimaye kupata msingi imara wa kuweza kuzijenga upya, ili ziwe katika mwelekeo ambao ni chanya. 

Ninatumaini kuwa, ukishakuwa umefahamu nini cha kufanya, basi utaweza kufahamu ni kitu gani unatakiwa kufanya na ni kwanini ni muhimu kwako.
Katika kuchunguza undani wa akiri yako na hatimaye kupanua dirisha lako la fikra zako, unahitaji kufikiria mambo 5 ya msingi:

1.      Jua Kuwa Maisha Yako, Yanatengenezwa na Fikra Unazozipa Kipaumbele Kila Siku.
Ukisoma kitabu cha Bwana James Allen kiitwacho “As a Man Thinketh” anatoa mafundisho ya kwamba, wewe binadamu ndiye unayetengeneza au kuharibu maisha yako mwenyewe kutokana na fikra juu ya fikra ulizonazo akirini mwako. Na pale unaporuhusu mawazo yatokee unakuwa ni muhanga wa maelfu ya mawazo hasi na imani finyu zinakuzunguka kupitia duara lenye taarifa hizo kila muda unaopita.

Unapokuwa mfikiriaji mahili wa mawazo (mtu mwenye kufikiri na kuchagua kile unachofikiria), basi jua kuwa hapo una uwezo wa kujenga maisha ambayo ni chanya na kutembea kila siku kuelekea kwenye ndoto yako ya maisha mazuri.

2.      Jua Kuwa Kubadili Kitu Chochote Nje ya Wewe, Lazima Ubadili Fikra Zako Kwanza.
Kama unataka watu wengine wabadili mtazamo wao wa jinsi wanavyochukulia au kukuona, lazima uanze kujibadili wewe kwanza. Kama unataka kubadili uchumi, jibadili wewe. Kama unataka kubadili hali ya maisha, jibadili wewe mwenyewe. Kama unataka kubadili dunia, jibadili wewe mwenyewe. Hiyo ndiyo kazi ya ndani yako ambayo utengeneza upenyo halisi na kuelekea kwenye mafanikio.

3.      Jua Kuwa Fikra Chanya Hazijengwi kwa Siku Moja.
Mwelekeo wa fikra ulizonazo ziwe chanya au hasi, zinajengwa ndani ya mzunguko wa siku 30. Baada ya siku 30 za kufanya kitu fulani, jua kwamba imekuwa tabia yako. Na maoni yako juu ya mwenendo wa maisha uliyonayo, pia ni matokeo ya tabia ya fikra zako za kila siku. 

Kwahiyo, usifanye kitu hiki siku ya Jumatatu peke yake na kutarajia kuwa millionia siku ya jumanne. Tambua kwamba ukiweka siku 30 za kufikiri mambo chanya fikra zako zitabadilika kwa kiasi kikubwa sana. Na baadae unapanda viwango kwenda hatua nyingine ya juu zaidi na kuendelea…

4.      Jua Kuwa Unatengeneza Maisha Mazuri kwa Kujenga Taswira Nzuri Mwenyewe.
Taswira yako inatengenezwa na picha ya iliyoko kwenye ubongo na ambayo inachezesha fikra zako kwa siku nzima. Ni jinsi gani unavyojiona wewe mwenyewe kufanikiwa au kutofanikiwa. Ndiyo sababu, jambo namba moja hapo juu ni muhimu sana.

5.      Jua Kuwa Kile Unachokiamini Ndicho Kinawezekana
Kama kweli unaamini unaweza kufanya chochote na ukafanyia kazi imani hiyo, basi kwa hakika utaweza kufanikisha ndoto yako. Ni lazima uamini kuwa unaweza kufanya kitu chochote. Unaweza kuimba kwamba “unaaamini unaweza kupaa,” lakini hauamini kwamba unaweza kufanya hivyo na kwahiyo, sheria ya uvutano bado inafanya kazi. 

Na inaweza kuwa kukuhamasisha ukajikuta unapendekeza kuwa unaweza kusogeza mlima kwa kutumia mbegu ya ndogo sana ya zao la ulezi, lakini wote tunajua kuwa hicho ni kitu ambacho hakiwezi kutokea. Lakini unapokuwa umeweka malengo, unaweza kwa dhati ukayatimiza kwa kwenda kuyafanyia kazi, na ikawezekana kuwa hivyo. Hakikisha kuwa unafanya kazi na kutimiza majukumu yako ya kila siku yanayohusu maendeleo yako binafsi.

Jitahidi kuweka fikra chanya na kujua kwamba sehemu yako ya ubongo inayoitwa subconscious itakuongoza wewe kuchukua hatua moja baada ya nyingine hadi kufanikisha hicho ulichokipanga kukifanya kuwa dhahiri. Endapo utakuwa umenielewa nazungumzia nini juu kuchukua hatua dhidi ya ya mambo 5 hapo juu, basi hapana shaka unaweza kuishi ndoto zako. Na hiki ndicho ninachokutakia ukifanye.

Mpendwa msomaji, endelea kuitumia vizuri MAARIFASHOP ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuwezesha kupata mafanikio. Ili kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza neno TUMA MAKALA MAARIFASHOP kisha sajiri barua pepe yako. Na kama unapenda kupata mafunzo ya kila siku kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO

Monday, October 19, 2015

Chimbuko la Umaskini kwa Waajiriwa ni Hili Hapa



  • Waajiriwa wengi wanauza nguvukazi ikiwa bado “ghafi”
  • Ukiuza nguvukazi ghafi umeuza “mtaji” na kuuza mtaji ni “kufirisika” jumla
Umaskini ndani ya kundi la wasomi unazidi kuingia kwa kasi ya ajabu kadili siku zinavyozidi kwenda. Kundi la watu ambao wako kwenye hatari kubwa zaidi ni hasa wale tulioko kwenye “ajira”. Ukweli ni kwamba watu wengi walioko kwenye ajira, kitu pekee wanachouza ili kupata kipato ni nguvukazitena ambayo bado ni “ghafi”.  

Uzoefu unaotokana na tafiti zilizofanywa, unathibitisha kuwa zipo sababu nyingi zinazosababisha waajiriwa na hasa wasomi wengi kuwa maskini. Lakini kubwa zaidi ni utamaduni wa wasomi kuendelea kuuza nguvukazi ikiwa bado ni “ghafi” (nguvukazi ambayo haijachakatwa). Katika ulimwengu wa “uwekezaji” nguvukazi ghafi ni mtaji muhimu sana, ambao ukichanganywa na mitaji mingine kama vile mashine, una uwezo wa kuzalisha bidhaa na huduma zenye thamani kubwa kwa watu wengine.

Ukiuza nguvukazi ghafi unakuwa umeuza “mtaji” wako: Waajiriwa wengi tumeendelea kukumbwa na adha kubwa ya umasikini kutokana na kushindwa kutambua ukweli kwamba mara nyingi kwenye maisha yetu ya ajira tumekuwa tukifanya zaidi biashara ya kuuza mtaji tulionao (nguvukazi) kwa matajiri wenye hitaji la mitaji.
Ikumbukwe kuwa, ili uweze kuzalisha bidhaa na huduma unahitaji mitaji ya aina mbalimbali ikiwemo nguvukazi ghafi. Ndiyo maana matajiri wengi wanapendelea zaidi kununua mitaji kwaajili ya kuzalisha bidhaa na huduma, ambazo huwapatia faida kubwa sana. 

Katika biashara yoyote duniani, kuuza mtaji ni kufirisika jumla. Kwahiyo, umasikini tulionao umetokana na kuuza mtaji wetu kila siku tunapotumikia ajira zetu. Kwa maana nyingine waajiriwa wengi tunafirisika kila siku ya Mungu tunapokwenda kazini.

Watu wanaouza zaidi nguvukazi ghafi wanabaki kuwa maskini kutokana na ukweli kwamba thamani ya nguvukazi ghafi huwa ni ndogo sana, kwasababu inapatikana kwa wingi na haina usumbufu kuipata. Kwa mfano: ukijifanya kutoza bei kubwa nguvukazi yako; waajiri wengi watakukimbia na chapuchapu watapata watu wengine wenye kuuza nguvukazi ile ile kwa bei nafuu sana.

Hivi ndivyo unavyouza nguvukazi ghafi: Unauza nguvukazi ghafi pale unapotumia nguvu yako kufanyakazi ya kuzalisha bidhaa na huduma ambazo siyo mali yako bali ni mali ya mtu aliyekuajiri (mwajiri). Unahitaji kufahamu kuwa, mwajiri amekuajiri ili umpatie (umuuzie) nguvukazi ambayo ni mtaji wa kuzalisha bidhaa na huduma ambazo ni mali yake binafsi. 

Kwakuwa bidhaa zinazozalishwa ni za thamani kwa watu wengine, basi ni wazi kwamba watu hao watampatia pesa mwajiri wako ili kupata bidhaa; LAKINI hawatakupatia pesa wewe, kwasababu wewe unayo nguvukazi peke yake, ambayo siyo hitaji muhimu kwa wateja wenye pesa zao. 

Ukiuza nguvukazi ghafi unauza “muda” wako: Kwakuwa umeajiriwa kwa madhumuni ya kutoa nguvukazi kwa mwajiri wako, basi thamani yako inapimwa kwa kuangalia muda unaoutumia kufanya kazi. Ili uweze kulipwa ni lazima kila siku ufike kazini na kusajiri muda wako. Usipoonekana kazini hakuna malipo yoyote, kwasababu muda wako utakuwa hujauwekeza kwa mwajiri. 

Kwahiyo, unapouza nguvukazi ghafi basi ujue umeuza “muda” na binadamu wa kawaida hawezi kufanya kazi zaidi ya masaa nane kwa siku. Masaa yote haya unafanya kazi bila kupumzika na kuzalisha vitu vyenye thamani kubwa kuliko mshahara unaolipwa na mwajiri wako. 

Haijalishi, thamani ya vitu vilivyozalishwa ni kubwa kiasi gani, mshahara wako unaolipwa unaendelea kubaki pale pale kila mwezi. Hali hii ndiyo inakufanya wewe mwajiriwa kukosa muda wa kufanya vitu vyenye kukuletea faida kubwa na mafanikio maishani, na hivyo kuzidi kuwa maskini kadiri umri wako unavyoongezeka.

Ukiuza nguvukazi ghafi huna cha kurithisha familia yako: Kama unauza nguvukazi ghafi siyo rahisi kuirithisha kwa watu wako wa karibu, kwasababu nguvukazi kama ilivyo haihamishiki kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Kama kitu hakihamishiki ni vigumu pia kukibadilisha kwa urahisi kuwa pesa.

Hali hii inazidi kutukumba wasomi na waajiriwa tuliowengi kutokana na ukweli kwamba unakuta umeajiriwa kwenye kampuni kubwa na una cheo kikubwa lakini ukifukuzwa au kufariki, haitokei mke au mtoto wako akapewa nafasi kama uliyokuwa nayo na wala familia haiwezi kutumia vyeti vyako vya elimu kuomba kazi. Lakini kama ungekuwa kwa mfano umeandika vitabu, hata ukifa hakimiliki ya kuendelea kuvichapisha na kuviuza inahamishiwa kwa warithi wako na wanaendelea kufaidi sawa na wewe ulivyokuwa ukifaidi.

Ukiuza nguvukazi ghafi unapata hasara: Hasara kubwa unayoipata kutokana na kuuza nguvukazi ni pale unapoishia kuuza kitu kimoja tu! Nacho ni nguvukazi. Hali hii inakubana kiasi kwamba unajikuta unalazimika kumtegemea mteja mmoja ambaye ni “mwajiri” na inakuwa siyo rahisi kubadilisha mteja kadiri unavyotaka.
Endapo ukiamua kuchakata nguvukazi yako na hatimaye kuzalisha bidhaa na huduma za thamani ni rahisi kupata wateja wengi, ambao ndio huleta mapato makubwa.

Hasara nyingine unayopata pindi unapouza nguvukazi ghafi ni kuendelea kubaki kwenye kundi la watu maskini ambao wanapata kipato hai (active income), yaani unapata pesa unapofanya kazi tu, ukiacha pesa hakuna. Endapo, ikitokea unaumwa au umesafiri basi ujue hakuna pesa itakayoingia.

Ndiyo maana unakuta mtu ni tajiri leo kwasababu anafanya kazi ya kibarua, lakini baada ya muda mfupi unakuta ni maskini na kwa waajiriwa ni hivyo hivyo wanakuwa na pesa wakiwa bado kazini LAKINI wanapostaafu ajira wanarudia kwenye hali ya umaskini jambo ambalo huwafanya watu wengi kufa miaka michache baada ya kustaafu.

Washindi dhidi ya umaskini ni wale walioamua kuchakata nguvukazi yao: Ukweli ni kwamba kila mchakato wowote lazima utoe matokeo. Matokeo ya kuchakata nguvukazi ghafi ni “bidhaa au huduma” zenye thamani kubwa kwa watu wengine. Kitendo cha kuchakata nguvukazi kinatokana na matumizi ya nguvu ya akiri pamoja na nguvu ya mwili kwenye rasilimali kama ardhi, maliasili, ujuzi, pesa n.k, kwa lengo la kupata mali au bidhaa kwaajili ya watu wengine. 

Ukishapata bidhaa zenye thamani (manufaa) kwa watu wengine, basi mara moja watakuletea pesa ili kujipatia bidhaa na huduma muhimu kutoka kwako. Kadiri utakavyotengeneza bidhaa nyingi na zenye thamani kubwa ndivyo utakavyopata pesa nyingi ambayo haina kikomo. 


Ni wakati sasa tuamke na tujibidishe sana kwa kuandaa mazingira yatakayotuwezesha hasa sisi wataka mafanikio kuuza “matokeo” ya nguvukazi badala ya utamaduni wa sasa wa kuuza nguvukazi ghafi. Ukweli ni kwamba, unapokuwa mtu wa kuuza matokeo ya nguvukazi ambayo ni bidhaa na huduma mbalimbali, tayari unakuwa umemaliza kazi, kinachofuatia ni kuendelea kuuza bidhaa hizo na wakati huo huo unakwenda kuwekeza muda wako huo kwenye kuzalisha vitu vingine, huku akiendelea kufaidi matunda ya kazi aliyoifanya mwanzo.

Kwa watu wote na hasa waajiriwa tunaotaka mafanikio makubwa, ni lazima kila mmoja wetu ajiwekee tarehe ya mwisho ya kuacha kuuza nguvukazi ghafi. Kila mmoja akifikia tarehe yake ya mwisho kuuza nguvukazi ghafi, mara moja aanze kujikita katika kubadili nguvu ya akiri na hisia kuwa bidhaa na huduma zenye kuwa suruhisho la kudumu kwa matatizo na changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wengine.

Kwakuwa utazalisha bidhaa na huduma zenye kuwa na manufaa makubwa kwa watu wengine, basi na wao watakupatia zawadi ambayo ni pesa, ili kujipatia kila kilicho bora kutoka kwako. Tukiweza kufanikisha azima hii, basi tutatajirika kutokana na ukweli kwamba watu wengi kwasasa wanataka bidhaa na huduma ambazo ni suruhisho ya changamoto zao. 
 
Wateja ni wengi ambao wako tayari kununua kila kitu kitakachozalishwa ilimradi kina thamani kwao ~ kwahiyo soko ni kubwa. Nchi yetu inapokaribia kuingia uchumi wa kati, mahitaji ya bidhaa na huduma zitokanazo na nguvu ya akiri/fikra zitazidi kuongezeka. 

Bidhaa zenyewe ni kama vile muziki, sanaa, vitabu, program za mafunzo ya ujasiriamali/biashara/afya/kilimo/majengo pamoja na machapisho juu miongozo mbalimbali ya uwekezaji katika mambo ya utalii, uwindaji, gasi, mafuta, madini, kilimo n.k.

Uchumi wa watanzania ukizidi kuongezeka na idadi ya wasomi ambao ndio wahitaji wakubwa itazidi kuongezeka huko tuendako ~ Kwahiyo ewe mtanzania mwenzangu, anza kuchukua hatua leo, wakati ni sasa.

Mpendwa msomaji, endelea kuitumia vizuri MAARIFASHOP ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuwezesha kupata mafanikio. Ili kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza neno TUMA MAKALA MAARIFASHOP kisha sajiri barua pepe yako. Na kama unapenda kupata mafunzo ya kila siku kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO