Ufunguo wa Pesa






Pesa ni kitu gani mpaka karibu kila mtu anaitafuta? Kama pesa inatafutwa na kila mtu, lazima kujiuliza wapi hasa inapatikana. Je? Ni kweli wote tunafahamu sehemu au mahali inapopatikana? Kama mahali pesa ilipo hapajulikani tutawezaje kuipata? Maswali yote haya yanahitaji majibu kwanza kutoka kwa kila mmoja wetu ambaye anazitaka pesa kwa dhati.

Maswali yote haya pia ndiyo yanatoatafsiri halisi ya kwanini kila mmoja anakwambia kuwa anahangaika kutafuta pesa, wengine wanakwambia siku hizi kuwa wanapambana. Yote haya yanaonyesha dhahiri kuwa kuna vita ndani kwa ndani katika fikra, akili na nafsi zetu juu ya wapi pesa itapatikana. 

Uzoefu unaonyesha kwamba mahali pesa ilipo bado hapajulikani kwa waliowengi. Kutokana na hali hii, wengi suala la kutafuta pesa linabaki kuwa suala la kubahatisha na kubangaiza. Kutafuta pesa kwa kubangaiza kumekuwa ndiyo hali ya maisha ya kila siku kwa waliowengi. 

Wakati ukiendelea kutafuta majibu ya maswali hapo juu, ni vizuri kutambua mambo makuu muhimu juu ya pesa; Moja ni kwamba, pesa halisi inapatikana ndani yetu; Pili, pesa yote unayoiona ni ISHARA tu ya kitu fulani kilichofanyika. 

Pesa inakuwaje ISHARA na kupatikana ndani yako? 

Nguvu ya hisia ikichanganyika na matamanio ndani ya akili, inaachia nguvu ya ubunifu wa vitu na huduma mbalimbali. 

Baada ya hapo akili yako inakusukuma ili ukamilishe kazi ya kubadilisha huo ubunifu uliopo katika hali ya wazo kuwa vitu halisi ambavyo mwisho wake hukuletea pesa. 

Ndiyo maana tunasema PESA ni ishara ya nguvu ya ubunifu ulionao katika hali ya kuonekana kwa macho. Kwahiyo, pesa tunatembea nazo mawazoni mwetu, tunalala nazo usingizini, tunakuwa nazo kila mahali tunapokua. 

Kazi tunayo moja tu nayo ni kuzitoa huko ndani yetu. Ili tuweze kuzitoa pesa ndani yetu tunahitaji kuendelea kujifunza namna bora ya kuzitoa nje, maana zikikaa tutakufanazo. 

Binadamu ukishapata kile unachohitaji na ukawa na uhuru wa kuchagua upate nini na uache nini ndiyo unapata kuishi maisha ya furaha na kuridhika pia. 

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba wewe umejaliwa nguvu ya ubunifu ndani yako na hiyo ndiyo hazina ya pesa uliyonayo. Kwahiyo, unatakiwa kuwa mtu mwenye matumaini na kuhakikisha hofu na mashaka havina nafasi kwako. 

Habari njema ni kwamba leo hii kuna idadi ya watu wengi sana ambao tunakaribia kuwa watu bilioni tisa hivi. 

Watu wote hawa wako tayari kulipa pesa ili kukidhi mahitaji yao. Unachotakiwa kufanya kama wewe ni kukidhi mahitaji ya asilimia ndogo sana ya watu wote walioko hapa duniani. 

Kwahiyo, ukiona umepata pesa ujue kuwa hiyo ni ishara inayoonyesha nguvu ya ubunifu ndani yako. 

Wengi wanaofikiri hawana pesa siyo kwamba hawana nguvu ya ubunifu tunayosema BALI ni kwamba hawajachukua muda wao kutambua kuwa nguvu hiyo ipo lakini pia hawajachukua hatua ya kuibadilisha nguvu hiyo kuwa vitu halisi vyenye thamani na ambavyo vinaweza kuuzika kwa watu wengine tukapata pesa. 

Kila wakati tuzame zaidi katika kutafiti na kufuatilia hitaji hasa la jamii tunayoweza kuifikia na katika hitaji lao hilo tuone pesa kwa macho yetu ya rohoni. 

Tukishaona kwa macho ya ndani tuanze kufanyakazi ya kuitoa ndani kwa maana ya kufanyakazi kwa vitendo ili kukidhi hitaji lililopo kwenye jamii husika. 

Kazi ya nguvu ya ubunifu ikishakamilika, watu wenye uhitaji wataleta pesa kwako na utaanza kuikusanya kwenye kapu, hapo ndio itaanza kuonekana kwa watu wengine. 

Baadae, utaanza kusikia watu mtaani wakisema fulani amezipata pesa, sijui amezitoa wapi wakati wao ndio wamezileta kwako….hivyo ndivyo maisha yanavyokwenda. 

Mpendwa msomaji wa makala hii litafakari sana suala hili la kuitoa nje pesa iliyoko ndani kwani ni rahisi kuutokomeza umaskini moja kwa moja. 

Najua unapenda kufuata njia za mkato lakini ukweli ni kwamba ukae ukijua kuwa pesa inayopatikana kwa njia za mkato inadumu kwako muda mfupi sana na wakati mwingine njia inayotumika siyo rahisi kuitumia wakati mwingine. 

Kwahiyo, wakati ukiendelea na njia zako za mkato anza taratibu kufuata kidogo kidogo njia hii ya nguvu ya ubunifu ili kutengeneza mfereji wa pesa zitiririkazo kuja kwako bila kikomo. 

Kwahiyo endelea kuitumia vizuri MAARIFASHOP ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuwezesha kuitoa nje pesa iliyoko ndani yako. 

Kupata mafunzo ya kila siku na makala mpya kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO

Kama unapenda kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza kiungo hiki; NITUMIE MAKALA kisha sajiri barua pepe yako.


Umuhimu wa Kutafuta Pesa Bila Sababu ni Huu


“Unashindwa kupata pesa nyingi kwasababu unatafuta pesa kulingana na shida unazotegemea kupata siku zijazo” ~ Cypridion Mushongi
Siku moja nilikuwa naongea na rafiki yangu ambaye aliwahi kuniuzia kiwanja siku za nyuma. Baada ya mwaka mmoja tangu rafiki huyo aniuzie kiwanja, tulikutana mjini Bukoba na hapa aliniuliza juu ya mpango wangu wa kukiendeleza kiwanja hicho. Jibu langu kwake lilikuwa...
“kwasasa sina pesa, ngoja kwanza nijipange”.

Jibu hili la kwamba mimi sina pesa halikumridhisha sana, ndipo akaniambia maneno mazito tena kwa lugha ya kihaya! “Amahela Geija Omubyemba!” Tafsiri isiyo rasimi kwa maneno haya ni kwamba “pesa uja wakati wa matatizo na shida”.

Shida na matatizo yanayozungumziwa hapa ni kama vile kuugua au kuuguliwa, kupatwa na msiba, harusi, kesi mahakamani, kudaiwa, karo za shule, ndoa kuvunjika n.k.

Tulipoachana nililazimika kuandika maneno yale kwenye kitabu changu cha kumbukumbu za kila siku. Wakati nikiendelea kundika nilizidi kutafakari kwa kina, juu ya jambo hili la pesa kupatikana wakati wa matatizo na shida. Nilizidi kujiuliza ni kwanini pesa ipatikane tu wakati tunapopatwa na shida au matatizo?

Bilashaka, maneno ya rafiki yangu huyu, yalilenga kunikumbusha kuwa, pindi nikiamua kwa dhati kuanza ujenzi, kwa vyovyote vile pesa itapatikana tu!.

Ukichunguza kwa kina, utagundua kuwa watu wengi ambao ni maskini ndani ya fikra zao, hawana na hawafikirii kuwa na pesa nyingi. Maisha ya maskini ni kana kwamba wakati ambao hakuna shida au matatizo, haoni haja ya kutafuta pesa!

Kwahiyo, kama hakuna shida, mara nyingi watu wengi uchagua kutokuwa na pesa. Kwa maana nyingine ni kwamba, watu wa namna hii wanapopatwa na shida, ndipo uanza kuona umuhimu na ulazima wa kutafuta pesa.

Kwa watu wa namna hii hasa maskini, shida na matatizo ndivyo vinakuwa sababu kubwa na kichocheo cha mtu kutafuta pesa kwa namna yoyote hile. – Pesa upatikana kwa muda mfupi!.

Katika hili tunajifunza mambo mengi, lakini mojawapo ni kwamba “watu wengi tunashindwa kupata pesa nyingi kwasababu hatujafikia hatua ya kutafuta pesa bila sababu zinazotokana na shida. 

Ukitafuta pesa baada ya kusukumwa na mahitaji ya matatizo pamoja na shida, basi ujue fika kuwa zikishapatikana zitatumika mara moja kwaajili ya kuondoa shida ambayo ndiyo ilikutuma uzitafute.

Matatizo na shida vikiisha na pesa inaisha. Pesa ikishaisha na wewe unaedelea kuishi maisha yako ya siku zote. Maisha ambayo umezoea kupata pesa ndogondogo basi!. 

Matatizo mengine yanapoibuka ndipo unaanza upya kujituma tena kutafuta pesa ili kukabiliana na shida zilizo mbele yako.

Imaonekana bila kuwepo sababu maalum na hasa inayotokana na shida/matatizo ya wakati huo, wewe hauko tayari kutafuta pesa. Kwahiyo, ni sawa na kusema “hakuna shida hakuna haja ya pesa”. Kwa maana nyingine ni kwamba, wakati ambao siyo wa shida, kutafuta pesa ni usumbufu. "Mtindo wa maisha ya namna hii ni hatari sana kwa maisha yako".

Watu wengi wanashindwa kupata pesa nyingi kwasababu, wanatafuta pesa kulingana na shida au matatizo wanayotegemea kupata siku zijazo. “Haya ni majanga”!
Watu waliofanikiwa (matajiri) mara nyingi utafuta pesa bila sababu zitokanazo na shida. Unapotafuta pesa bila sababu ya matatizo na shida unakuwa na wakati mzuri wa kufikiria na kuendeleza miradi mikubwa na yenye tija kwa watu wengi. Hii ina maana unatulia na kutafuta pesa bila kukurupuka -Yawezekana ndiyo maana matajiri wana pesa nyingi.

Ikumbukwe kuwa, kila kitu afanyacho binadamu anakuwa na sababu. Lakini, jiulize, wewe unatafuta pesa kwasababu gani? Aina ya sababu ndiyo itakufanya ama upate pesa nyingi au upate pesa kidogo sana.

Sababu ya maskini kutafuta pesa ni kumaliza shida/dharura, majanga aliyonayo. Lakini, watu matajiri utafuta pesa ili kuzidi kupata vitu vingi na utajiri kwa ujumla. 

Kwahiyo, ndoto, malengo, sababu, dhamira n.k. ya kutafuta pesa ndizo zinatofautiana kati ya mtu na mtu. Kwa maana hiyo, wewe ndiye wa kubadilisha malengo na sababu ya kutafuta pesa.

Mpaka hapa ni kwamba, kama wewe ni mmojawapo wa watu wanaotafuta mafanikio, ni lazima uwe mtu wa kutafuta pesa bila ya kusukumwa na sababu zitokanazo na shida/matatizo. Jitahidi kujituma sana kutafuta pesa ikiwezekana jitume kuliko yule atafutaye pesa kwasababu ya shida na matatizo.

Sasa umeyajua haya! Ni lazima tuanze pamoja kutafuta pesa bila sababu zitokanazo na shida/matatizo.

Hatujachelewa hata kidogo tuanze leo.

Kwa maoni zaidi au ushauri jiunge NA mtandao huu kwa kubonyeza neno hili: MAARIFA SHOP.


Siri ya Faida Kuwa Bora Kuliko Mshahara Imefichuka
“Lengo la biashara yoyote ni kutoa suruhisho ya matatizo ya watu-kwa FAIDA” ~ Paul Marsden
Pesa ambayo huwa tunapata mara zote utoka kwenye mifumo mikuu miwili ambayo ni “mfumo wa mshahara” na “mfumo wa FAIDA”. Kati ya mifumo hiyo, mfumo wa mshahara ndio unaotegemewa na kuaminiwa na watu wengi. Lakini pia ndio mfumo ambao unazalisha maskini wengi, na ni mfumo ambao watu wake uhangaika sana kutafuta pesa ya kujikimu.

Watu ambao huwa wanafanikiwa kupata uhuru wa kipato au pesa ni wale ambao wanapata pesa yao nyingi kutoka kwenye mfumo wa faida kuliko wale wanaotegemea pesa kutoka kwenye mfumo wa MSHAHARA.

Kwa wale wote ambao tunapata pesa kutoka kwenye “mfumo wa mshahara”, biashara yetu kubwa ni ya “KUUZA MUDA” kama ulivyo. Kama unamiliki mfumo wa faida, unaweza kuwekeza pesa yako tena na tena katika mfumo huo huo na hatimaye kupata pesa nyingi.

Mfumo wa mshahara unakupatia pesa mara moja kwa kipindi Fulani kilichopangwa. Mfano kwa waajiriwa wegi serikalini pamoja na makampuni makubwa ya binafsi, pesa inatoka mara moja kwa mwezi nje ya hapo hupati kitu hata kama una shida kiasi gani hakuna namna.

Wakati huo huo, mfumo wa faida unakuwezesha wewe kupata pesa kila siku. Unapoweza kupata mapato (pesa) kila siku inakusaidia kufikia ulinganifu wa mapato na matumizi.

Ukweli ni kwamba, watu wengi tunaopata pesa yetu kutoka kwenye mfumo wa mshahara tunakabiliwa na tatizo sugu la kutokuwa na ulinganifu wa mapato na matumizi yetu. Kutokuwepo kwa ulinganifu wa mapato na matumizi ndiko kunasababisha watu wengi kutumia zaidi kuliko mapato yao halisi.

Mfumo wa mshahara unatufanya tupate pesa mara moja kwa mwezi na wengine kama wakulima ni baada ya miezi miezi 4 hadi 6. Mfumo huu wa kupata pesa mara moja baada ya kipindi kirefu ndio unatufanya watu wengi kukabiliwa na mzigo wa madeni yasiyoisha.

Hali hii ndiyo inatufanya wengi hasa waajiriwa kushindwa kupata mitaji ambayo ingetuwezesha kuingia kwa urahisi kwenye “mfumo wa faida”. Kwa maana nyingine ni kwamba tayari tumejenga tabia au utamaduni wa kula bila ya kuwa na pesa.

Kitu kinachoitwa mshahara au ujira huwa siyo cha kudumu, muda wowote kinaweza kukoma. Inatosha kusema kwamba, maisha ya mshahara yanakutaka usiugue/usiuguze, usisafiri n.k. 

Kwa maana nyingine ni kwamba ukisimama kufanya kazi, pesa nayo inakatika hapo hapo. Pesa yako itakoma au kushuka kama utakuwa unaumwa. Pale utakapostaafu, pesa yako itapungua..ingawaje unataka pesa nyingi hasa pale unapostaafu

Hatahivyo, kama utajikita na kuegemea zaidi upande FAIDA , badala ua mfumo wa mshahara basi ataweza kutengeneza pesa wakati akiwa amesinzia au huko kwenye gym n.k. Endapo akiugua bado atatengeneza pesa nyingi. ukistaafu, pesa yako itaendelea kama kwaida.

Maisha ya mshahara siyo rafiki kwa maana hayatoi mwanya kwako wewe kuweza kufanya shughuli au mambo yale unayoyapenda. Mfumo wa mshahara unatumia zaidi ya asilimia 90 ya muda wa mwajiriwa. 

Kama mwajiriwa huna udhibiti wowote wa mshahara wako wa kila mwezi. Wale wanaokulipa ndio wanaojipangia wakate ushuru kiasi gani bila hata ya kukuuliza.

Siku zote waajiri wako wanakata pesa yao kwanza, alafu wanakupangia kiasi utakachotumia kuendesha maisha ambayo wao wanaona ni muhafaka kwako. Kimsingi maisha yako yote yanadhibitiwa hadi unakosa kuifurahia dunia hii yenye maziwa na asali.

Kwa ufupi ni kwamba mfumo wa mshahara unakusaidia tu! wewe upate kuishi LAKINI mfumo wa faida unakusaidia wewe kutajirika…jambo ambalo ni zuri zaidi.

Uzoefu umeonyesha kuwa hakuna mtu yeyote ambaye huwa anatajirika kwenye mfumo huu wa mshahara. Labda wanamichezo au wanariadha wachache wenye majina makubwa. Wengine ni wakurugenzi wa makampuni makubwa ambao pamoja na kuuza muda wao, pia, utajiri wao mkubwa unatoka kwenye mfumo wa faida kupitia mikataba yao, kwa mfano kuwekeza na kupewa kiasi fulani cha hisa za makampuni wanayoyaongoza.

Njia pekee ya kupata ukombozi na uhuru wa kipato ni kila mara wewe kutenga kiasi fulani kutoka kwenye mshahara wako, ili kuwekeza pesa hiyo kwenye “mfumo wa faida” kama biashara ya hisa, ardhi ya kukodisha, nyumba ya kupangisha, biashara ya kushirikisha rafiki zako taarifa za bidhaa au huduma (jenga mtandao) n.k. hapo utakuwa tayari kwenye mfumo wa faida.

Ili kupata usalama na uhuru wa kipato, ni wakati muhafaka sasa wa kutoka kwenye “mfumo wa kuuza muda” ili upate pesa yako na kwenda kwenye “mfumo wa faida”.

Ewe mtanzania, muda wa kuanza jitihada za kuingia na kupata pesa kutoka kwenye mfumo wa FAIDA ni leo. Ni muda muhafaka pia wa kuanza kujiuliza maswali magumu. Kwa mfano: inabidi ujiulize; utakuwa wapi miaka 10 ijayo, endapo utaendelea kukaa kwenye mfumo wa mshahara?, je? Ukiendelea kufanya biashara ya kuuza MUDA, utaacha miaka 10 ipite bila kutimiza malengo yako?

Kuna mengi ya kuzungumza kuhusu jinsi ya kuhama kutoka kwenye mfumo wa mshahara kwenda kwenye mfumo wa faida. LAKINI nimeona ni vizuri wewe msomaji wa MAARIFA SHOP, … ukatoa maoni yako juu a dhana hizi mbili yaani MSHAHARA na FAIDA……Endelea kutoa maoni juu ya hili…


Unajua Kwanini Pesa ni Ngumu Kupatikana?

“Kutokuwa na pesa ni chanzo cha mabaya mengi” ~George Bernard Shaw.


Binadamu ili apate kufahamu kitu fulani lazima picha iliyoko kichwani ilingane na kufanana na kitu unachotafuta. Endapo picha zikipishana lazima itakuwa vigumu sana kupata hicho unachotafuta. Mara nyingi, tizo hili la kupishana kwa picha linatokea zaidi kwa vitu vingi ambavyo siyo....
halisi, kama vile PESA. Katika suala la pesa, watu wengi wanapicha ambayo haiendani na uhalisia wa pesa yenyewe. Kwa maana nyingine ni kwamba pesa, siyo kitu halisi tofauti na inavyochukuliwa na watu wengi.
Kitu ambacho siyo halisi, mara nyingi huwa hakioneani kwa urahisi mpaka utumie macho ya ubongo ndipo unaweza kukiona. Kwa maana nyingine ni kwamba pesa ni kitu ambacho akionekani kwa macho, na ni kitu ambacho SIYO HALISI. 
Watu wengi wanadhania kuwa pesa ni kitu halisi, ndiyo maana wakiona zile noti na silver wanadhani wameona pesa…hapo kila mmoja utakuta anafukuzia ufukuzia noti lakini bila mafanikio yoyote.

Inatosha kusema kuwa katika utafutaji wetu wa pesa tuko katika makundi makuu mawili ya watu. Kundi la kwanza ambalo ndilo la wengi ni lile linaloichukulia pesa kuwa ni kitu halisi na mara nyingi hawa wanatumia HISIA zaidi katika kufanya maamuzi mbalimbali juu ya utafutaji wake. 
Kundi la pili ni lile la watu wachache ambao wanaitambua pesa kama “kitu ambacho SIYO HALISI ~ ni WAZO” na mara nyingi wanatumia ukweli katika kupanga na kuchagua njia za kuitafuta pesa.

Mara nyingi kundi ambalo linadhania kuwa PESA NI KITU HALISI, imekuwa vigumu sana kwao kupata pesa endelevu na wakati mwingine wameweza kuzikosa kila wanapoweka mtego. Kama usipochukua muda wako kutafakari juu ya pesa, ni rahisi sana kushawishika na kuona kile unachokiona kwa macho kama kitu halisi.

Hatari ya kuiona pesa kama KITU HALISI ni pale unapoifunga akiri yako isiweze kuona na kujua kile kinachosababisha pesa kuingia mfukoni. Kwakuwa akiri yako itakuwa tayari imejifunga basi mwisho wake ni kwamba hautajali kuboresha au kuendeleza kile ambacho kinakuwezesha wewe kupata pesa hiyo unayoifurahia sasa.

Kwa upande mwingine ni kwamba, ukiweza kuitafakari pesa katika uhalisia wake basi utaipata bila wasi wasi wowote, kwani kila mara utashikiria sana kile ambacho huivuta pesa kuja kwako.

Nitamjuaje mtu ambaye anaichukulia pesa kama kitu halisi? Ni wazi kuwa umewahi kuwasikia watu wengi wakisema kuwa pesa ni sabuni ya roho, pesa ni kila kitu, pesa ni bahati, siri ya kupata pesa aijulikani n.k. Hisia za namna hii juu ya pesa ndizo zinawafanya watu wengi kupenda kutumia njia za mkato ilimradi tu wamezipata.

Utumiaji wa njia za mkato katika kutafuta pesa umesababisha madhara mengi sana kwenye jamii zetu hizi hasa za kitanzania ambazo hazijawa na mifumo imara ya kijamii. Tumekuwa tukishuhudia wizi wa pesa, watu wanadhurumiana, watu wamejenga chuki na ndugu na jamaa na mengine mengi.

Madhara mengine ni ya kiuchumi kama kaya na taifa kwa ujumla…Watu wengi wanaodhania pesa ni kitu halisi siyo rahisi kwao kuamini katika kuzalisha vitu na huduma (thamani). 
Wengi wanakuwa hapa katikati au mwishoni mwa ule mnyororo mzima wa uzalishaji. Mwisho wake bidhaa na huduma zinakuwa chache sana kiasi cha watu wengi kushindwa kuzipata kutokana na bei yake kuwa kubwa.
Nchi ambayo ina watu wengi wa namna hii, mara nyingi inategemea sana bidhaa kutoka nje ambazo tumeshuhudia kuwa ni feki (bei rahisi) jambo ambalo limefanya thamani ya shilingi ya Tanzania kushuka kila siku.

Watu wengi wakizidi kuamini kuwa pesa ni kitu halisi, ni wazi kwamba siku zote wataendelea kuamini kuwa pesa walizonazo ni kidogo na mwisho kujikuta wakijenga wivu na chuki dhidi ya wale wanaowadhania kuwa wanazo pesa nyingi.

Falsafa yangu katika hili ni kwamba “Ukidhania pesa ni kitu halisi, basi ujue kuwa hata njia na mbinu utakazotumia kutafuta zitakuwa zinafanana na zile za kutafuta vitu halisi”.

Kwa kawaida, upatikanaji wa vitu vyote ambavyo ni halisi huwa ni wa moja kwa moja; unatumia mchakato mfupi kuvipata. Ukitaka kitu fulani, ni kiasi cha wewe kunyanyuka na kufuata kilipo. Pia, vitu vyote ambavyo ni halisi, michakato yake ya kuvipata huwa ni rahisi sana na hauhitaji kufikiri sana.

Mfano: Ukitaka nyanya moja kwa moja ama utaenda shambani kwako au utaenda gengeni hayo yakifanyika unapata nyanya kwa dakika chache. Ukihisi njaa moja kwa moja unatafuta kitu halisi ambacho ni chakula – ama utakwenda nyumbani au hotelini, michakato hiyo ikifanyika tayari tatizo lako la njaa litakuwa limekwisha.

Kwahiyo, inaonekana faulo yetu ya kwanza katika kutafuta pesa ni pale tunapotumia mbinu ambazo ni maalum kwaajiri ya kutafutia vitu halisi.

Vitu ambavyo siyo halisi kama ilivyo pesa, navyo vina utaratibu wake na mbinu zake katika kuvitafuta. Pia ni vizuri kukumbuka kuwa, pesa yoyote unayoiona siyo halisi bali ni kitu kilichopewa thamani na binadamu, japokuwa pesa ni muhimu sana katika maisha lakini akili, afya na ufahamu wako ni muhimu kuliko PESA. Maana pesa ulipwa baada ya kuzalisha thamani (kutoa vitu na huduma).

Kwa maana nyingine ni kwamba, thamani yoyote ile uzalishwa au kuendelezwa na wewe binadamu. Wewe ndie unayetoa huduma au kuzalisha, wewe ndie unayechagua kazi gani ufanye ili upate pesa, hivyo wewe ni zaidi ya pesa na wewe ndie unayeamua upate pesa nyingi au kidogo. Lakini yote hayo yatategemea sana wewe kuacha kuiona pesa kama kitu halisi.

Kwahiyo, inahitajika wewe mwenyewe ufikirie kwa kina hadi ujiridhishe pasipo shaka lolote kuwa PESA SIYO KITU HALISI. Endapo utakuwa umekubali wewe binafsi tokea ndani mwako, basi tuungane katika kufahamu na kujifunza mbinu na njia mpya zinazotumika katika kutafuta na kupata vitu ambavyo siyo halisi kama PESA. Kwa kujielimisha kila siku, tutakuwa tumejenga uwezo wetu wa kutafuta na kupata pesa nyingi bila kuzikosa.


Unadhani Pesa Uliyonayo ni Kidogo au Nyingi?
"Mungu hakupi pesa kidogo au nyingi, anakupa tu kile kiasi unachohitaji”.



Kwasasa wapo watu wengi wanaodhani kuwa wao wanazo pesa kidogo na wangependelea Mungu awaongezee. Pia kuna wale wachache ambao wanadhani wanazo pesa nyingi lakini na hawa wangependelea Mungu azidi kuwapa pesa nyingi zaidi. Ki-ukweli hakuna pesa kidogo wala pesa nyingi.

Ukimwambia mtu yoyote kuwa “pesa aliyonayo ni sawa na kiasi unachohitaji”, anakukatalia kata kata kwasababu, hisia zake zinamtuma kuamini kwamba yeye ana pesa kidogo na mpaka anafikia hatua ya kulaumu watu wegine anaodhani wana pesa nyingi.

Katikati ya mwezi wa December mwaka 2015 nikiwa kwenye likizo yangu ya mwaka nilikutana na rafiki yangu ambaye ni Mganda Bw. Sam Mpiira. Rafiki yangu huyu ni mjasiriamali anayechipukia jijini Kampala-Uganda.Tukiwa tumekutana kwenye viunga vya hotel ya Speak Resort Munyonyo, tuliongelea sana juu ya namna tunavyoweza kutajirika na hatimaye kusaidia watu wengine kutajirika. Katikati ya mazungumzo yetu alinieleza mojawapo ya falsafa yake kuhusu “KUPATA PESA” na hapa alisema “Mungu hakupi pesa kidogo au nyingi, anakupa tu kile kiasi unachohitaji”.

Ukiangalia kwa undani unaona kuwa Falsafa hii inatugusa wengi, na inatuonyesha umuhimu wa kuacha kulichukulia suala la pesa kuwa la HISIA, badala yake tuone ukweli juu ya pesa tuliyonayo kuwa ni matokeo ya fikra na jitihada zile tunazoziweka kila siku basi!. Endapo tukilitabua hilo basi tutakuwa tumeachana na fikra za kwamba kupata pesa ni “bahati”.

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa watu wengi bado wana machungu na wanalalamika kila wakati kwamba wao hawafanikiwi kupata pesa ya kutosha. Kuwepo kwa hali ya malalamiko juu ya pesa kidogo kunaonyesha dhairi kuwa ufahamu uliopo ni kidogo, kwasababu mfumo wa elimu ya darasani hauna ajenda ya kufundisha pesa. Na pia watu wengi tumefanya utafutaji wa pesa kuwa wa HISIA zaidi kuliko ukweli ulivyo.

Ndugu msomaji wa MAARIFASHOP, siri unayotakiwa kuijua leo ni kwamba, suala la kiasi gani cha pesa huwenacho ni la binafsi zaidi kuliko unavyofikiria. Hali hii inatokana na uwepo wa mahitaji yanayo tofautiana kati ya mtu na mtu. Ni vigumu kwangu mimi kufahamu wewe una kiu kiasi gani ya pesa. Utofauti huu wa mahitaji ya pesa ndio uzaa shauku, nguvu, motisha na hamasa tofauti linapofika suala la kutafuta pesa. 

Kwahiyo, wale ambao ndani ya nafsi zao wana sababu nzito ya kutafuta pesa ndio wanapata kiasi hicho ambacho kwako wewe uliye na sababu nyepesi unaona wamepata pesa nyingi. Napenda kurudia tena kusema kuwa “hakuna aliye na pesa nyingi bali kila mtu anacho kiasi ambacho ni hitaji lake kwa wakati huo”.

Kwahiyo, kila mtu kabla ya kuanza mchakato wa kutafuta pesa ni vizuri ukatenga muda wa kutafakari kwanza juu ya maisha yako wewe binafsi.Tafakari zako zielekeze kwenye vitu vizuri ambavyo ungependa kuwa navyo maishani au hali ya maisha ambayo unadhani ukiifikia utajisikia raha na mwenye furaha.

Kwa maana nyingine lazima huwe na picha au ndoto ya maisha mazuri kwanza kabla ya kuyafikia. Ndoto ya maisha mazuri ndiyo itakayo kujengea sababu na hamasa ya wewe kutafuta pesa ya kutimiza ndoto yako. Utaratibu wa namna hii, utakusaidia sana kuachana na malalamiko. Pia ukiwa na ndoto yako ya maisha mazuri itakuwa vigumu kuwaonea wivu watu wengine waliotimiza ndoto zao, yaani wale ambao sasa hivi unadhani wana pesa nyingi.

Kikubwa hapa ni kufikiri, kutafakari, kupanga na kutekeleza kwa vitendo. Ninaamini kama pesa ndiyo shida yako itapatikana tu japo itachukua muda. Ni muhimu kutokata tamaa na kuwa mvumilivu.

Kama unadhani ni muhimu kuwa na mawasiliano ya karibu na mtandao huu wa “MAARIFA SHOP”, ni kiasi cha kubonyeza maneno haya “KARIBU MAARIFASHOP, -tayari utaanza kupata moja kwa moja mambo mapya ya mtandao huu.

  
“Falsafa ya matajiri na masikini ni hii hapa: Matajiri wanawekeza pesa yao na kutumia kiasi kinachobaki, Masikini wanatumia pesa yao na kuwekeza kiasi kinachobaki” ~ Robert Kiyosaki
 
Hali ya umaskini katika jamii yetu kwa kiasi kikubwa imesababishwa na watu wengi kuuza muda wao kwa watu wengine. Dunia ya leo bado inatawaliwa zaidi na kundi la watu ambao biashara yao ya kila siku ni kuuza muda kwa lengo la kujikimu kimaisha. Katika ulimwengu wa kutafuta riziki (kipato), tunapata kuona aina kuu tatu za kipato ambazo ni.....

kipato kutokana na ajira, kipato hai na kipato endelevu au kipato bila kikomo.

Karibu asilimia 90% ya watu duniani wanapata kipato chao kutoka kwenye ajira (mshahara) na kujiajiri (mapato hai). Ni chini ya asilimia 10% pekee ndio wanapata aina ya kipato abacho hakina kikomo –kikianza kuingia kinaendelea hata kama haupo kufanya kazi. Kwa maana nyingine ni kwamba, asilimia chini ya 10% ndio matajiri wanaomiliki asilimia 90 ya utajiri wote duniani.

Kimsingi mapato yanayotokana na kujiajiri (kipato hai) na ajira, yote ni mapato ambayo tunayapata baada ya “kuuza muda wetu” au kubadilishana muda (mwajiriwa) na pesa (mwajiri). Kutokana na hali hiyo ya kuuza na kununua muda, ndiyo maana watu wengi tuliokwenye ajira au tuliojiajiri mara nyingi hatuna muda wa kufanya vitu tunayovipenda hata kama vina maana na umuhimu mkubwa kwetu.

Kwa maana nyingine ni kwamba muda mwingi ambao tungeutumia katika kubuni vitu vipya tunakuwa tumeishiwa tayari kutokana na ukweli kwamba tumekwisha uza muda huo kwa watu wengine hasa waajiri –zaidi zaidi tunafanya biashara ya kuuza muda basi!

Kutokana na ukweli wa mambo ulivyo ni kwamba wauzaji wa muda kama mali tuko wengi sana kuliko wanunuzi (waajiri). Matokeo yake ni kwamba soko la MUDA linashuka au tuseme bei ya muda inashuka kila kukicha. Hali hii imetufanya wote wauza muda kuuza kwa bei ya chini ambayo hailingani na thamani ya kitu tunachokiuza. Leo hii, tunashuhudia migomo ya kila aina hasa kwa wafanyakazi wa viwandani na mashambani, hoja yao kubwa ikiwa ni maslahi duni au mishahara midogo “Kiduchu” isiyoweza kukidhi hata mahitaji ya lazima kama vile chakula na malazi.

Nataka kupata MAPATO YASIYO NA KIKOMO lakini siyajui ni kitu gani:
Unapoongelea suala zima la mapato yasiyo na kikomo ni sawa na wewe kufunga bomba la maji mtoni, ili kuleta maji nyumbani kwako. Maji yakishafika nyumbani wewe unayatumia unavyotaka na hayakatiki. Wale wote wasiofikiwa na mabomba ya maji majumbani mwao, wao wanachokifanya ni kuchota maji kwa kutumia vifaa kama ndoo, madumu n.k.

Watu hawa wakishapata maji, wanayatumia na inafika wakati yanaisha. Mara tu maji yanapoisha, inawabidi wafunge safari tena kwenda kuchota maji popote yalipo, na mzunguko unakuwa hivyo maisha yao yote. Ukichota maji yanakuwepo nyumbani, usipochota maji hayapo LAKINI yule mwenye bomba anaendelea kupata maji masaa yote, hata akiwa amesafiri maji yapo tu!.

Mfano huu wa maji ni sawa na mfumo wa mapato tunayoyapata. Kwa maana nyingine ni kwamba, wale wote tunaopata mapato hai au mapato ya ajira (mshahara), tunafanana kabisa na wale watu wanaochota maji mtoni kila siku kwa kutumia ndoo, madumu n.k. Kwa mfano: Mapato ya ajira -unalipwa siku unapofanya kazi, usipofanya kazi haulipwi, ukisafiri bila ruhusa haulipwi, ukiugua muda mrefu hulipwi n.k.

Kwahiyo, mapato bila kikomo ni mapato anayopata mtu pasipo kuwa na ulazima wa kushughulika au kufanya kazi kwa wakati huo. Mapato haya mara nyingi yanatokana na kazi au shughuli uliyokwisha kufanyika kitambo na kuendelea kupata mapato hayo “kimya kimya”, kutokana na ukweli kwamba watu wengine wanakuona tu umekaa lakini kumbe wewe unaingiza pesa nyingi mfukoni.

Kwa tafsiri nyingine ni kwamba mapato au pesa isiyo na kikomo ni ile ambayo mtu huipata mara kwa mara, lakini kwa kutumia nguvu kidogo sana katika kuiendeleza. Mfano; ni pesa itokanayo na haki miliki kama;k.m. pesa ya mrahaba au “royalties” kutokana na kuuza vitabu, album au kukodisha hakimiliki; faida benki; kodi ya majengo au mashine; au pesa kutoka kwenye biashara ambayo haikuhitaji tena wewe kuwepo moja kwa moja kama “biashara ya kupashana habari au mtandao”. Hii ni mifano tu ya vyanzo vya pesa isiyo na kikomo. Aina hii ya mapato inapatikana baada yaw ewe kufanyakazi kwa bidii sana kwa muda fulani (k.m. miaka 2 hadi 5), baadae unaendelea kupata pesa kwa muda mrefu bila hata wewe mwenyewe kushughulika tena au zaidi.

Uzuri wa mapato yasiyo na kikomo ni kwamba, unaendelea kupata pesa kwa muda mrefu baada ya kazi ya uzalishaji au ya awali kukamilika. Hali hii ya wewe kupata pesa bila kulazimika kufanya kazi tena ndiyo ukuwezesha wewe kupata MUDA wa ziada na hivyo kupata fursa ya kuwekeza muda huo kwenye mambo mengine. Uzuri mwingine wa mapato haya ni kwamba duniani kote hayatozwi kodi kubwa kama mapato ya aina nyingine.

Kwa wale wote tulio na ndoto ya kupata mafanikio makubwa kimaisha tunashauriwa kufanya kazi na kuwekeza kwenye miradi inayotuhakikishia kupata mapato yasiyo na kikomo. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mapato ya aina hii, ndiyo mapato pekee ambayo ni imara, endelevu na yanarithishwa kizazi hadi kizazi. Sababu nyingine inayonituma nikushauri kupata mapato haya ni kwamba, watu wengi waliofanikiwa (matajiri) duniani, wamejipanga na kujikita katika kupata mapato haya.

Je? unawezaje kutumia mapato yasiyo na kikomo kununua tena muda wangu? Je? kununua muda wako tena kuna maana gani? Maana yake ni kwamba pesa ambayo unatengeneza kwa wiki kutoka kwenye biashara ambayo ni zaidi ya pesa uliyokuwa ukipata ulipokuwa ukimfanyia kazi mtu mwingine (mwajiri). Kwa upande mwingine, mapato bila kikomo yana tabia ya kununua muda wako tena kwakuwa yanarudisha kwako ule muda au masaa yote uliyokuwa ukiyatumia kufanya kazi za mwajiri.

Inapotokea biashara yako ikaanza kukupatia kipato kikubwa kisicho na kikomo na ambacho ni zaidi ya pesa (mshahara) uliyokuwa unaipata kutokana na kuuza muda wako kwa mwajiri, basi hapo utakuwa hulazimiki tena kuuza muda wako ili kupata mahitaji na badala yake hayo masaa yako uliyokuwa ukibadilishana awali na pesa, sasa unaanza kuyatumia (kuyawekeza) wewe mwenyewe katika kukuza faida na hatimaye kujijengea mikondo mingi ya kuingiza pesa –hii ndiyo namna ya kujenga utajiri.

Ukiona biashara au shughuli yako unayofanya inakuletea pesa isiyokuwa na kikomo, basi ujue kuwa biashara hiyo inaweza kukusaidia kununua muda wako na hatimaye ukajimilikisha tena muda huo. Kwa mantiki hiyo, ni wazi kwamba mapato yasiyo na kikomo ndiyo pekee yanaweza kukuwezesha wewe kurudisha au kununua tena muda wako.

Mwisho nipende kusema kuwa utakapoamua kwa dhati kujifunza undani wa mapato yasiyo na kikomo utakuwa ni sawa na mtu aliyepata dhahabu au aliyepata kujua suala nyeti. Kutokana na unyeti wa mapato ya aina hii, ndiyo maana ninapenda sana watu tuliowengi tuyafahamu na kuyajua kwa undani zaidi.

Tukisha elewa vizuri dhana nzima ya mapato yasiyo na kikomo; ni matarajio yangu kuwa tutaweza kuhama kutoka mfumo wa biashara ya kuuza muda (mshahara) kwenda biashara ya kuwekeza muda (faida). Nakusihi uanze mchakato wa kujifunza hatua wa hatua kupitia makala nzuri za ujasiriamali na mafanikio nyingi zikiwa zinapatikana hapa kwenye mtandao wa “MAARIFA SHOP”. Kama unapenda kuwa karibu na mtandao huu bonyeza KUWA KARIBU.

Kwa mawasiliano zaidi:

WhatsApp: 0788 855 409

E-mail: mchumieconomist2009@gmail.com

Tovuti: http://maarifashop.blogspot.com


Unataka Kutajirika Anza na Hili 
“Uhuru wa kipato upo kwa wale tu waliotayari kujifunza na kufanya kazi” ~ Robert Kiyosaki
Watu wengi wanatafuta utajiri kwa hudi na uvumba, japo wengine wachache wanapata na waliowengi wanakosa na kukata tamaa. Jambo ambalo ni dhairi kabisa ni kwamba, watu wengi tunaanza safari ya kutafuta utajiri katika hatua au vituo tofauti tofauti. Kwahiyo, swali la kujiuliza ni je? Safari yetu ya kutafuta Utajiriinapaswa kuanzia...
wapi?.

Katika utafiti na uzoefu wangu nimegundua kwamba, UTAJIRI unaanzia kwenye fikra. Na “fikra ni nguvu pekee inayoweza kuzalisha utajiri wa kuonekana kutoka kwenye vitu visivyoonekana”. 

Kila kitu unachokifanya sasa hivi kimeanza kama wazo kutoka ndani yako. Hakuna matendo utakayotenda bila kuanzia kwenye fikra (mawazo).

Kwahiyo, ukiwaza kwa namna fulani, basi ujue kwamba utapata utajiri wa namna fulani sawa na ulivyowaza mwanzoni kabla ya kupata utajiri huo. Fikra au mawazo, ndio kitu pekee ambacho huweza kukusukuma kufanya vitu fulani fulani ambavyo ndivyo huweza kukuletea utajiri.

Utajiri sio dhambi, bali ni sehemu ya maisha, tumeletwa hapa duniani kuweza kutawala vilivyopo na kama ukiweza kuvitawala vizuri ni lazima utakuwa tajiri. Unachohitaji ni kuweza kugeuza ndoto yako kuwa kweli.

Wakati ukifanya yote hayo, kumbuka kuwa, wewe ni mtu mwenye thamani kubwa sana isiyokuwa na mwisho. Hata kama unajiona wewe sio mtu mbunifu, hata kama ulishashindwa huko nyuma, hata kama unafikiri umeshajaribu kila kitu ila ukashindwa, jua kwamba bado una nafasi kubwa ya kupata chochote unachotaka.

Huwezi kuishi maisha unayoyataka, huwezi kuishi maisha yenye uhuru kama huna utajiri. Huwezi kuinuka na kufikia juu kwenye chochote unachofanya kama kweli huna uhuru wa kipato.

Ndio maana ni muhimu sana kwako kuwa TAJIRI. Kwa kawaida binadamu wote tunazo nia tatu ambazo tunaishi nazo, yaani mwili, akiri na roho. Nia hizi ndizo utengeneza maeneo muhimu ambayo utuongoza kuishi ama maisha ya utajiri au maisha ya umaskini.

Maeneo hayo yote matatu ni muhimu sana katika kuishi maisha yenye mafanikio na furaha. Ni lazima mwili uwe na utajiri, akili iwe ya utajiri na roho pia iwe na utajiri, hapo ndipo itawezekana wewe kuifikia ndoto yako ya utajiri.

Lengo la maisha yetu ni maendeleo yaletwayo na utajiri na wala si kitu kingine. Msingi mkuu wa maisha ni kuendelea kupiga hatua. 

Kama kila kitu kwenye maisha kinakazana kuwa zaidi ya kilivyo sasa, iweje wewe leo uendelee kuwa pale pale miaka yote? Mti unakazana kukua zaidi ya ulivyo sasa. 

Na wewe binadamu pia ni lazima ukazane kuwa bora zaidi ya ulivyo sasa katika maeneo yote muhimu ya maisha yako.

Katika harakati zako za kutafuta utajiri, lazima kuhakikisha kuwa fikra zako zinakuwa safi muda wote. Unatakiwa kutumia nguvu ya utashi wako kuzuia akiri yako isirishwe mambo ya umasikini, na ifanye akili yako ibaki imeshikiria imani na kusudi la maono ya kile unachotaka kufanya au kuumba .

Kamwe usizungumze: Jitahidi usizungumzie kuhusu matatizo yako ya zamani ya kifedha kama ulikuwa nayo; usiyafikirie kabisa.Usizungumze kuhusu umaskini wa wazazi wako au ugumu wa maisha yako ya huko nyuma. Kufanya lolote kati ya hayo ni kujiweka kiakiri katika umaskini kwa wakati huu ulionao sasa.Weka umsakini na mambo yote yanayohusiana nao kado au nyuma yako kabisa.

Linda mazungumzo yako: Kamwe usizungumze kuhusu masuala yako au chochote kile katika namna ya kuvunja moyo au kukatisha tamaa. Kamwe usikubali uwezekano wa kushindwa au kuzungumza katika namana inayoashiria kushindwa. Unatakiwa kutozungumza kuhusu nyakati kuwa ngumu au mazingira ya biashara kama vile una mashaka.

Nyakati zinaonekana kuwa ngumu kwa wale wote walio katika usawa wakushindana na wenzao. Lakini, wewe unayetafuta utajiri wako hunabudi kuanza kujifunza maisha yale ambayo unashindana na malengo yako au ndoto zako basi. 

Mwisho lakini siyo kwa umuhimu nipende kusema kuwa Mafanikio ni mchakato siyo tukio. Kwahiyo, kama wewe umeweza kujifunza kitu chochote kipya na cha thamani kutoka kwenye makala hii ni wazi kwamba tayari umeanza mchakato wa kuelekea mafanikio. 

Kitu kikubwa kingine unachoweza kufanya ni kuwashirikisha marafiki zako wanaopenda kujifunza namna bora ya kufanikiwa na hapa wanahitaji tu kubonyeza neno “NITUMIE MAKALA MPYA”.

 

 

 

Sababu ya Wewe Kutopata Mtaji Imebainika

Ukipata pesa na ukaitumia kabla ya kutenga akiba, basi ujue umelipa watu wengine kwanza na wewe umesahau kujilipa”
Tajiri mkubwa na mashuhuri duniani, Bwana Warren Buffet aliwahi kusisitiza kuwa, kama unataka kujenga mtaji kutoka kwenye akiba yako binafsi ni sharti ujitahidi kuacha tabia ya “kuweka akiba baada ya kutumia na badala yake utumie kile kinachobaki baada ya kutenga pesa ya akiba”. Katika maisha ya umilikaji pesa duniani, kuna makundi ya ina mbili. 

Kundi la Kwanza ni la wale wanaoweka akiba ya kile kinachobaki baada ya wao kutumia na kundi la pili ni wale wanaoweka akiba kabla ya kutumia.  Kwa mfumo wetu wa mapato na matumizi ya pesa, tunaona kuwa kundi la waweka akiba baada ya kutumia ni wengi sana na ndilo kundi la watu ambao ni walalamikaji juu ya ukosefu wa mitaji ya kufanyia biashara au shughuli nyingine za kiuchumi.

Katika ulimwengu wa biashara, mtaji ndilo suruhisho la uwekezaji wowote wenye tija. Hatahivyo, mtaji umekuwa ni  adimu kuupata na umekuwa ni kikwazo namba moja cha watu wengi kushindwa kuwekeza na hatimaye kuwa wajasiriamali. Ili kuweza kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa mitaji, watu wengi wamezidi kuhamasishwa kujiweea akiba binafsi kidogo kidogo kutoka kwenye mapato wanayopata. 

Lakini pamoja na kwamba njia hii ya akiba binafsi ni rahisi na ya uhakika, bado suala la kuweka akiba limekuwa gumu kutekelezeka. Sababu kubwa ya kushindwa kujiwekea akiba ni kwamba watu wengi tumejenga utamaduni wa “kutumia kwanza na akiba baadae”. 

Ukweli ni kwamba, pindi tunapopata pesa, kitu cha kwanza kufanya ni kutumia kwanza kwa lengo la kumaliza eti shida zilizopo. Hapa kipaumbele kinakuwa ni kumaliza shida na siyo kuweka “akiba”. Uzoefu umeonyesha kuwa, ukipata pesa na ukaanza kutumia kabla ya kutenga akiba, inakuwa siyo rahisi kubakiza pesa yoyote kwasababu shida ni nyingi na mahitaji ya wakati huo ni  mengi, ukilinganisha na kiasi cha pesa unachokuwa umepata. 

Ukipata pesa na ukatumia kabla ya kutenga akiba, basi ujue umelipa watu wengine kwanza kabla ya kujilipa wewe. Utamaduni wa kulipa watu wengine kwanza pindi tupatapo pesa umezidi kukua siku hadi siku na tumeendela kuulithisha kwa watoto wetu. Pesa yoyote unayojilipa kwanza ndiyo hiyo hugeuka kuwa “akiba”. Tunahitaji kujenga utamaduni wa kujilipa kwanza kabla ya kufikiria kununua kitu chochote kile pindi tunapoingiza pesa mifukoni mwetu.

Nimeshindwa kujiwekea akiba kwahiyo…. Kwakuwa nimeshindwa kujijengea nidhamu ya kuweka akiba ili hatimaye nipate mtaji, basi nimeamua kwenda kukopa mtaji ili nianzishe biashara yangu. Maeneo ambayo watu wengi ukimbilia ili kupata mikopo ni pamoja na ndugu, jamaa na marafiki; mabenki, n.k. 

Hatahivyo, utumiaji wa mikopo kama chanzo cha mitaji, bado haujaweza kuwanufaisha kwa kiwango walichotarajia. Hii ni kutokana na upungufu mkubwa wa elimu juu ya mtiririko wa pesa (inayoingia na kutoka) au uelewa mpana juu ya mapato na matumizi ya pesa.

Kukosekana kwa uelewa wa kutosha juu ya utunzaji na utumiaji wa mikopo, wanufaika wengi wa mikopo, wamejikuta wakigeuka kuwa mawakara wa kudumu wa mabenki ya biashara. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, mikopo mingi imekuwa ikitumika zaidi kununua vitu ambavyo si vya kuingiza pesa mfukoni (assets), bali vimekuwa ni vitu vya kupeleka pesa nje ya mfuko. 

Wapo watu wengi ambao tumeshuhudia wakishindwa kabisa kurudisha mikopo na hapa wakopeshaji wa pesa, wanalazmika kunadi mali zao na hivyo kujikuta wakifirisika ghafla. Lakini chanzo cha kushindwa kurejesha mikopo kukosekana kwa nidhamu ya matumizi ya pesa ambayo haikujengeka huko nyuma. Bila kuwa na nidhamu na tabia ya kujilipa kwanza kutokana na mapato yako binafsi, huwezi kuwa na nidhamu ya kutumia pesa ya mkopo (ambayo siyo ya kwako) kwa umakini unaostahili. 

Kwahiyo, tabia ya kutenga akiba kabla ya kutumia (kulipa watu wengine), ndio inatuwezesha kujenga nidhamu ya matumizi stahiki ya pesa yetu binafsi na hata ile ya mkopo.

Akiba binafsi imeshindikana….! Wengi wetu tunashindwa kabisa kujiwekea akiba binafsi licha ya kwamba tunapata pesa ya kutosha. Kila wakati tunapopata pesa kitu cha kwanza tunachowazia na kukipa kipaumbele ni “MATUMIZIyaani kununua mahitaji (kuwalipa wengine) na pesa inayobaki ndiyo mara nyingi watu ukumbuka kujiwekea akiba. Haipiti wiki moja, ile akiba tuliyoweka mwanzoni baada ya kutumia nayo tunaitumia kwa mambo mengi ambayo ufanyika kwa mtindo wa dharura. 

Suala la kupenda kutumia haliishii hapo bali watu wengine uenda hatua ya mbele zaidi ambayo ni ya kutumia vitu  kwa mkopo ambapo mtu ulipa pesa baadae baada ya kupata pesa. Unapomkuta mtu yuko busy anatafuta pesa, husidhani mtu huyo anasukumwa na kutaka kutoka kimaisha laasha! Bali huyo mtu anatafuta pesa za kulipia madeni ya vitu alivyokwisha tumia siku za nyuma. 

Kwahiyo, itoshekusema kuwa mtu huyo alikula bila kufanya kazi, na adhabu yake ni kwamba matunda yote ya kazi yake, lazima yalipe madeni tu maana hamna namna nyingine.

Unapanga mipango ya kutumia baada ya kupata pesa? Tabia hii ya kutumia kwanza na akiba baadae ndiyo inawafanya watu wengi kuamini kwamba huwezi kupanga mipango yoyote kabla ya kupata pesa. 

Watu wa namna hii kwa kipindi ambacho hawana pesa wanakaa tu bila kupanga na kufanya chochote cha maana. Kwa maana nyingine, watu hawa bila kusukumwa na pesa waliyonayo mifukoni hawawezi kufanya jambo lolote la maendeleo. Hii ni hatari na lazima umaskini huwe halali yako.

Iwapo msukumo wako wa kufanya kitu chochote unategemea au kusukumwa na pesa tasilimu uliyonayo mfukoni ni wazi kwamba ikishapatikana, lengo la kuweka akiba kwanza haliwezi kupewa kipaumbele au wakati mwingine haliwezi kufanyika kabisa. 

Matokeo yake ni kwamba kila wakati utajikuta hubakizi chochote kwasababu kila mara utakapopata pesa, lazima utaipangia kulipia mahitaji (lipa wengine) alafu itaisha. Hali hii itakapoendelea na baadae kuwa tabia yako basi uje kuwa kila wakati wewe utakuwa ni mtu wa kukosa nidhamu ya kujiwekea akiba ambayo ndiyo ingezaa mtaji wa kutimiza ndoto zako. 

Waliofanikiwa wanaweka akiba kwanza kabla ya yote: Kwakuwa akiba binafsi ndiyo chanzo cha uhakika wa kupata mtaji binfsi, ni lazima tuanze kubadilika kwa kuanza kujifunza tabia ya wale watu waliofanikiwa. 

Watu waliofanikiwa, mara nyingi wanapopata pesa yoyote hile, kitu cha kwanza kwao huwa ni kutenga kwanza asilimia fulani ya pesa kama akiba na baada ya hapo ndipo ufikiria suala la matumizi mengine. Unapoweka akiba kwanza kabla ya kitu chochote ndipo unaweza kudhibiti tamaa yako, kwa maana utatakiwa kuwa na nidhamu ya kutumia kulingana na kile kilichobaki. 

Kwahiyo, jijengee tabia ya kutanguliza kujilipa kwanza kabla ya kulipa watu wengine; kwani kwa kufanya hivyo, utapata mtaji wa kutosha na hatimaye kufikia mafanikio makubwa maishani.

Ili kuendelea kupata makala hizi moja kwa moja kupitia e-mail yako bonyeza KUPATA MAKALA



UNASHANGAA NINI? PESA YAKO NI SANAMU

  • Ukitumia macho ya ubongo  unaona "Wallet" zetu hazijabeba pesa, bali vitu tofauti
  • Ikiwa biashara yako wewe ni kufuga na kuuza kuku, “basi elfu kumi yako ni kuku”
Ilikuwa siku ya jumanne ya tarehe 30/06/2015, kwenye kipindi cha tuongee asubuhi kinachorushwa na ITV kila siku mara baada ya kusoma magazeti asubuhi. Zamu hii, alikuwa akihojiwa kiongozi mmoja wa dini, ambaye alikuwa akijaribu kuelezea jinsi walivyojipanga katika kuandaa na kukamilisha siku ya mkesha wa kuombea uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka huu, na akasisitiza kuwa maombi yatafanyika mkesha wa 8/8/2015. Katika mazungumzo yake akagusia jambo moja muhimu kuwa kwa sasa watu wengi wanatanguliza pesa mbele hata kabla ya kufanya kazi na wengine wanadai walipwe pesa, ndipo wapige kura za ndiyo kwa wagombea, hasa katika kipindi hiki tunapoelekea uchaguzi mkuu. Kiongozi huyu, alitumia fursa hiyo kuwahasa watanzania kujiepusha na tabia ya kupenda kutanguliza pesa mbele. Katika kuweka msisitizo wa kuonyesha ni kwa jinsi gani pesa siyo kitu halisi; alirejea maandiko kutoka katika vitabu vitakatifu yanayosema kuwa “Pesa ni Sanamu”. Kitendo cha watu wengi kushindwa kutambua usanamu uliopo juu ya pesa, ndicho chanzo cha kuwepo kwa changamoto nyingi zinazotukabili leo hii kama watu binafsi na taifa kwa ujumla.

Dhana hii ya “pesa ni sanamu” ni muhimu tukaijua na kuielewa vizuri,  ili hatimaye mimi na wewe tupate kujinusuru kwa kutoka kwenye kundi kubwa la watu wanaotafuta pesa kama “sanamu”. Yawezekana leo hii hatupati pesa ya kutosha na unaangaika sana, kwasababu fikra na mitazamo yako ni ile ile ya kudhania kuwa pesa ni kitu halisi kumbe ni “sanamu”. Tafsiri ya neno “pesa ni sanamu” inamaanisha kwamba, pesa siyo kitu halisi bali ni mfano au kivuli cha bidhaa na huduma mbalimbali, ambazo hazionekani kwa macho yetu ya kawaida. Kwa maana nyingine, pesa ni kitu ambacho husimama badala ya bidhaa na huduma mbalimbali hasa wakati wa zoezi zima la ubadilishanaji vitu kati ya muuzaji na mnunuzi.

Usanamu wa pesa unatokana na ukweli kwamba, pesa uliyonayo mfukoni imetokana na wewe kuwapa watu wengine bidhaa au huduma ulizokuwa nazo; na wao kwa hiari yao wakaamua kukupa vithibitisho ambavyo ni kama stakabadhi zinazothibitisha uwepo wa makabidhiano ya bidhaa/huduma kati yako na watu wengine. Kwahiyo, unapoangalia pesa uliyonayo mfukoni ujue una mfano tu wa vitu vilivyofanya pesa kiasi fulani ije kwako. Kwenye wallet zetu hatuna pesa bali tuna vitu tofauti tofauti. Mfano: utakuta mtu mwingine kwenye wallet yake ameweka huduma ya mapambo, usafiri, ufundi, elimu, kuchangia mawazo kwenye vikao n.k. Wengine wallet zao utakuta bidhaa kama vile chakula, nguo, dawa, jiko, taa, simu, mafuta n.k. Ukiamua kutumia macho ya ubongo wako utakubaliana na mimi kuwa, pesa tulizonazo kwenye wallet zetu hazifanani.

Wote tunaweza kuwa na noti ya shilingi elfu kumi za kitanzania, ambazo kwa macho ya kawaida zinafanana, lakini kwa macho ya ubongo, wallet zetu hazijabeba pesa bali zimebeba vitu tofauti mtofauti kabisa. Kwahiyo, ikiwa wewe biashara yako ni kufuga na kuuza kuku basi elfu kumi yako ni kuku; kama wewe ni mwandishi basi elfu kumi yako ni habari, gazeti au kitabu na ikiwa wewe ni mshereheshaji basi elfu kumi yako ni ushereheshaji, ualimu, uchoraji n.k. Mifano hii michache inatuonyesha kuwa, pesa zote tulizonazo hazifanani kabisa, isipokuwa bidhaa na huduma tunazozalisha ndizo hubadilika na kuwa kitu kimoja ambacho ni sanamu yaani “pesa” inayoonekana kwa macho yetu ya kawaida. 

Kwa wale wote wanaoamini kuwa pesa siyo sanamu, maana yake ni kwamba vitu vyote vinavyotengeneza pesa waliyonayo, hawawezi kuviona kwasababu macho yao ya ubongo yamepofuka na hivyo wamebakia kutumia macho ya kawaida peke yake. Ukiangalia pesa kwa macho ya kawaida (kwa mujibu wa kinachonekana), kiukweli wewe utaishia tu kuona noti za elfu 10, 5, 2, 1 n.k. ikiwa kuona kwako kutaishia hapo, basi na wewe ni mmojawapo wa watu hawaoni pesa bali wanaona “sanamu”. Mtu anayeona sanamu kila wakati, hawezi kujua mahali kitu halisi kilipo na wala hatajua hiyo pesa ilikotoka. Ndiyo maana inapotokea mtu akapata pesa na baadae kuishiwa, ni vigumu kuzipata tena kwa haraka kwasababu, anakuwa tayari ameishasahau zilikotoka. Na kwa yule anayetambua kuwa pesa aliyonayo kwenye wallet ilitokana na mkusanyiko wa bidhaa na huduma mbalimbali; ni rahisi sana kwake yeye kuzipata pesa kwa muda mfupi, kwasababu chanzo chake kinajulikana na kimekuwa kikitunzwa na kuimarishwa mara kwa mara.  

Kwenye jamii yetu kwasasa, bado watu wengi wanaishi kwenye ulimwengu wa vitu vinavyoonekana kwa macho ya kawaida. Tunahitaji kujifunza kutumia macho yetu  ya ubongo katika kuona vitu vinavyoonekana na visivyooekana na hapo ndipo tutaweza kuiona pesa halisi badala ya sanamu tunayoiona sasa. Ni wakati muhafaka sasa kwa watu wote wanaotaka mafanikio makubwa kugeukia kile kinachofanya pesa ije kwenye wallet zao; kwani hicho ndicho kitu halisi. Ni muhimu, juhudi na maarifa yetu yote yakaelekezwa kwenye kuzalisha thamani kupitia vitu na huduma mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya watu wengine na jamii kwa ujumla. Na tuyafanye yote haya, huku tukiamini kufanikiwa na hakika tutafanikiwa.


PESA NYINGI INAPATIKANA HAPA
  • Unapoamua kuwekeza nguvu kazi yako kwenye shughuli za uzalishaji ndipo unapata bidhaa.
  •  Unapokuwa na bidhaa/huduma ndipo watu wengine sasa huamua kutoa na kutuma pesa zao kwako, ili kujipatia bidhaa/huduma husika.

 Leo hii watu wengi tunahangaika, tunanungunika na tunalalamikiana juu ya kukosekana kwa pesa. Kila mtu anamtuhumu mwenzie juu ya hali duni ya maisha. Maisha duni yametokana na kukosekana kwa mahitaji. Ili binadamu apate mahitaji, kwa sehemu kubwa anahitaji pesa na hii mara nyingi inatokana na bidhaa au huduma ambazo umezalisha mwenyewe. Uzalishaji wa bidhaa au huduma zilizonyingi unategemea zaidi matumizi ya nguvukazi, ambayo chimbuko lake ni afya bora. Mtu mwenye afya bora, kwa vyovyote vile ni mtu mwenye kuwa na nguvu yakutosha kufanya shughuli mbalimbali na hasa za kiuchumi. Nguvukazi hatupewi na mtu yeyote, bali unakuwanayo kwa kuzaliwa ilimradi, uwe na utaratibu wa kujali afya yako basi!.

Kwakuwa kila mmoja wetu anamiliki na kuitawala nguvukazi yake mwenyewe, maamuzi ya kutumia nguvukazi yako kwa mtu mwenyewe. Kuna kundi la watu wanaotumia nguvukazi yao zaidi kwenye “Uzalishaji Pesa” na kuna wengine wanaitumia zaidi kwenye shughuli ambazo siyo za uzalishaji wa pesa (Non Income Generating Activities ~ NIGA). Hapa Tanzania, bado watu wengi wanawekeza nguvukazi kubwa zaidi kwenye shughuli zisizo za uzalishaji pesa. Shughuli nyingi ambazo siyo za uzalishaji pesa, zinatumia sana pesa, hali inayopelekea watu wengi kutumia kuliko wanavyozalisha pesa. Kama nguvu-kazi yetu nyingi inawekezwa zaidi kwenye shughuli ambazo siyo za uzalishaji, basi tujue kabisa kuwa tutapata bidhaa/huduma kidogo, na hatimaye tunaishia kupata pesa kidogo.

Watu wengi tunataka na tunatamani sana “maisha bora”; maisha ambayo tutakuwa na uwezo endelevu katika kupata chochote tunachohitaji kama lilivyo kusudio la Mungu kutuweka hapa duniani. Kwakuwa, maisha bora ndiyo kusudio la watu wengi, basi inatupasa tubuni mchakato wa maisha bora badala ya hali ya sasa ambayo tumejikita kwenye shughuli za kutafuta pesa ambazo hazina mpangilio. Kwa sasa ukichunguza harakati nyingi za kutafuta pesa, unagundua kuwa kila shuguli inajitegemea kiasi kwamba kukamilika kwa shughuli moja hakuna uhusiano wowote na shughuli nyingine. Jambo hili la kufanya shughuli ambazo hazina mpangilio maalumu unaolenga kupata maisha bora, ndiyo linatufanya tukose mwelekeo na hatimaye kushindwa kuyafikia maisha ya ndoto yetu. Kwahiyo, zoezi la kutafuta pesa na hatimaye maisha bora ni lazima kulifanya kuwa la ki-mchakato zaidi kuliko ki-shughuli zaidi. Kupitia fikra, utafiti, vitabu na hitoria za watu waliofanikiwa; nimejifunza kuwa, ili uweze kuyafikia maisha ya ndoto yako (maisha bora) ni muhimu upitie mchakato maalum. Mfano ni kama huu hapa chini:

AFYA BORA     NGUVUKAZI     BIDHAA     PESA     MAHITAJI     MAISHA BORA

Ukichunguza mchakato wa kupata pesa hapo juu unaona moja kwa moja kuwa pesa siyo matokeo ya mwisho ambayo binadamu anayatafuta bali pesa ni sehemu tu ya mchakato wa maisha bora. Katika mchakato wa kupata maisha bora, pesa ipo katika nafasi ya nne kati ya vitu sita muhimu ambavyo vinahitajika kupewa kipaumbele kama unataka kufanikiwa. Mafanikio makubwa yameshindikana kufikiwa na watu wengi, kwasababu ya kutilia mkazo zaidi kitu kimoja tu! ambacho ni PESA. Michakato yetu mingi ya kutafuta pesa, haitilii mkazo vitu vingine kama “afya, nguvukazi na bidhaa”. Kwa maana nyingine tunaweza kusema kuwa hatupati pesa kwasababu mara nyingi mchakato wa kutafuta pesa na hatimaye maisha bora “tunauanzia katikati”.

Unapopanga mkakati au mchakato wa kutafuta pesa na wakati huo huo ukaacha kuzingatia na kujali afya yako, basi ujue kuwa uwezekano wa wewe kupata maisha bora ni mdogo sana. Kumbuka afya bora ndio chimbuko la nguvu ulizonazo ambazo ndio hukupatia rasilimali “nguvukazi”. Unapoamua kuwekeza nguvu kazi yako kwenye shughuli za uzalishaji ndipo unapata bidhaa au huduma ambazo hugeuka kuwa pesa. Unapokuwa na bidhaa/huduma ndipo watu wengine sasa huamua kutoa na kutuma pesa zao kwako, ili kujipatia bidhaa/huduma husika. Kwahiyo, iwapo utakuwa umezalisha bidhaa nyingi utapata pesa nyingi na ni pesa hiyohiyo ambayo na wewe utaitoa na kuituma kwa watu wengine ili kupata bidhaa/huduma na hatimaye kukidhi mahitaji yako mbalimbali. Unapofikia hatua ya endelevu wa kupata kile unachohitaji kwa muda muhafaka, ni wazi kwamba unakuwa tayari umefikia maisha bora ambayo ni ya ndoto yako na hapa ndipo unaanza kupata vitu vile ulivyokuwa ukivipenda lakini ulilazimika kuviacha kwa muda ili kuruhusu mchakato wako wa maisha bora ukamilike.

Kwahiyo, tunapojiandaa kuanza safari ya kutafuta mafanikio ni lazima tujitahidi kuanza mchakato wa kutafuta maisha bora, kwa kuanza na ujenzi wa afya bora, ili itupatie nguvukazi itakayo tuwezesha kuzalisha bidhaa za kuleta pesa nyingi kukidhi mahitaji kwa kiwango endelevu na  hatimaye kufikia maisha bora ambayo ndiyo ndoto yetu.






USIBANE MATUMIZI YA KIPATO “TUMIA KIPATO KUPANUA NJIA ZA KUINGIZA KIPATO”


Yawezekana unaendelea kuishi maisha duni, kwasababu unaishi kwa “kubana matumizi”; na hii ni kutokana na ukweli kwamba, tangu tukiwa wadogo tumefundishwa na wazazi, ndugu jamaa na marafiki kuwa ili uweze kuwa salama ni “Ishi Chini ya Uwezo Wako”. Watu wengi wenye mtazamo huu, mara nyingi wanaotumia njia ya kubana matumizi kuwa ndiyo suluhisho na njia pekee ya kukabiliana na ugumu wa  wa maisha. Ukweli ni kwamba, kubana matumizi ni utaratibu mzuri lakini inategemea una malengo gani ya kufanya hivyo. Kutokana na kutotambua ubaya wa tabia ya kubana matumizi, wengi wamelichukulia kuwa ni utaratibu wa kudumu badala ya kuwa wa muda tu!. 



Watu wameendelea kubana matumizi tangu wanajitabua mpaka wanazeeka. Unapokuwa mtu wa “kubana matumizi” muda wote, kinachojitokeza ni kwamba unajenga hofu kubwa ndani yako juu ya kuishiwa pesa kidogo uliyonayo. Akiri yako yote inaelekezwa kulinda pesa yako isitoke au wengine wanasema eti! Itoke kwa mpangilio – lakini mwisho wa yote hali inabakia palepale “kuishiwa na kutaabika”. Kwa mtu ambaye amejiwekea utaratibu wa kudumu wa kubana matumizi, akiri yake inadumaa sana kiasi cha kukubali kuishi maisha duni na ufukara. Mtu wa namna hii kila anapotafuta na kupata, badala ya kuwaza ni kwa namna gani atapata kingi zaidi, yeye mara moja unawazia kuishiwa, ndiyo maana anaanza kuweka nguvu nyingi kubana hicho kidogo kilichopatikana. Mwisho anatumia kwa kujinyima sana na hatimaye kinaisha ndipo huyo mtu uhanza tena kutafuta. Kwahiyo, unajikuta umenasa katika mzunguko wa kuishiwa na maisha yanakuwa ni ya kubangaiza miaka yote. 




Kuishi chini ya uwezo wako ni kitu cha kawaida na mara nyingi ushauri utolewa sana na wataalam na wasomi wa masuala ya biashara na uchumi kuwa njia pekee ya kuendana na hali ni kufanya vitu vilivyo chini ya au vinanavyolingana na uwezo wako. Lakini badala ya kulikubali hili bila kulitafakali ngoja tujiulize ni kwanini wanasema hivi? Au kwanini imani hii ya kubana matumizi inatokea? chimbuko la kubana matumizi ni kuazia wakati ule wa zama za kale ambapo binadamu aliishi kwa kukusanya matunda na kuwinda wanyama. Wakati huo, watu hawakuwa na fikra za uzalishaji, kwasababu walizoea kula vitu ambavyo vilijiotea na kukua vyenyewe bila kutegemea akiri na nguvu ya binadamu.

Kazi ya binadamu wakati huo ilikuwa ni kutafuta na pale vilipopatikana vilikusanywa kiasi cha kutosha. Baada ya kuvikusanya, binadamu huyo wa kale alijitahidi sana kuvitunza ili vikae muda mrefu bila kuisha. Kwakuwa vitu hivi mara nyingi vilikuwa vinatoka mbali sana na makazi yao, ilibidi kujitahidi kubana ili kupunguza safari za kwenda huko; njiani walipambana na wanyama wakali, mafuriko, mvua n.k. kwahiyo kila walikuwa wakifkiria safari ilikuwa ni budi wabane kupunguza hadha za namna hiyo. Sasa wewe unayeishi katika zama hizi za leo, tayari una uwezo wa kuzalisha bidhaa na huduma mbalimbali, na hivyo kutotarajiwa kuishi kwa style kama ya enzi za kale. Uhamuzi ni wako kwa maana kwamba unaweza kuamua kuzalisha vingi na ukatumia kiasi unachoona kinafaa kukutoshereza mahitaj yako ya wakati huo. Badala ya kila wakati kufikiria kubana matumizi na mwisho kuishia kuishi katika maisha ya kupata mahitaji chini ya kiwango chako halisi.

Kuishi chini ya uwezo wako ni sawa a kujiaminisha kuwa suluhisho la kumudu gharama za maisha ni kupunguza matumizi. Kuishi juu ya uwezo wako ni sawa na kujiaminisha kuwa pesa ipo nyingi. Hali zote mbili hazifai, bali suluhisho pekee ni kupanua na kuongeza vyanzo vya mapato. Kila mmoja anaweza kupunguza matumizi, na kila mmoja anaweza kutumaini na kuomba Mungu kuwa pesa itakuja, lakini inahitaji ubunifu, maarifa na uelewa, pamoja na ujasiri ili kukuza na kupanua mapato yako kupitia njia halali. Kimsingi siamini katika kuishi chini ya uwezo na wala kuishi juu ya uwezo, ninachoamini ni kuishi kwa kupanua na kuongeza njia za kuleta mapato.
Siamini katika mtazamo wa “ishi chini ya uwezo wako”.  Kwa watu walio wengi pamoja na wale watoa ushauri, huu kwa ujumla ni mtazamo wa kimaskini na siyo mzuri. Lakini pia, kibaya zaidi ni kwamba ushauri huu wa kuishi chini ya uwezo unasababisha kuua kabisa dhamira na fikra za ujasiriamali. Ushauri huu unakufanya usinyae kuwa mdogo. Hali hii inafanya mtu anakuwa na maisha duni kuliko alivyopaswa kuwa. Hali hii pia inakufanya kuingia katika kundi la watu wa kawaida au wenye mawazo ya wastani (mediocre). Na kama uliwahi kuambiwa na wewe mwenyewe kuwazia kwamba unatakiwa kuishi chini ya uwezo wako acha mara moja. Huu ni wakati wa kukua na kufanya mambo makubwa, ni wakati wa kuwekeza asilimia kubwa ya kipato chako kwenye vitu vinavyoingiza pesa kwako; ni wakati wa kuwa mbunifu na kupanua siyo tu njia za kuingiza kipato, bali pia jitanue kwa kuilisha akili yako ili uweze kufaidika na fursa zilizokuzunguka.
 
NI VIGUMU SANA KUFANIKIWA KAMA MARA NYINGI UNAITUMA PESA YAKO KUNUNUA VITU NA KUBAKIA HUKO BILA KURUDI


Mara zote ukishakupata pesa (kuingia mfukoni), kinachofuata huwa ni kuzitumia hata kama ukizitunza kwanza, mwisho wake huwa ni kutumika kwaajili ya kukidhi mahitaji ya vitu na huduma mbalimbali. Watu wengine upenda kusema kwamba “pesa ni mzunguko”. Mzunguko wa pesa una vipengele viwili ambavyo ni “Kuingia na Kutoka”. Kwa lugha rahisi tunaweza kusema kuwa pesa ina milango miwili, kuna mlango wa pesa kuingia na kutoka kwako.



Kwa yeyote anayetafuta mafanikio makubwa ni lazima kuangalia milango hii miwili (kuingia na kutoka) na hapa ndipo kuna tokea makundi mawili ya watu ambao ni masikini na tajiri. Kwa upande wa maskini tayari wamejenga hofu kubwa sana na muda wote wana wasiwasi ya pesa kutoka na kupotea. Kutokana na hofu hii, maskini wengi sana wemejijengea tabia ya kuibana pesa ikisha ingia mifukoni mwao, huku wakidhani kuwa hilo ni suluhisho la wao kutoishiwa na pesa. Matokeo yake linapokuja suala la kuwekeza au kuchangamkia fursa kubwa wanakuwa waoga sana wa kuthubutu kutokana na hofu ambayo imejengeka kwa muda mrefu ndani ya fikra zao.



Wenzao ambao ni matajiri wao, mara tu pesa inapoingia, kitu cha kwanza ujiuliza ni kitu gani wanaweza kukitoa ili kuondoa kero kwenye jamii ikiwemo le iliyowazunguka. Kwahiyo, wao uweza kuiachia pesa yao kutoka lakini kwa malengo ya kuituma malighafi ambayo pengine ikiunganishwa na mambo mengine uweza kurudi na bidhaa au Huduma ambayo ni hitaji muhimu kwenye jamii. Kwa kufanya hivyo, hata wale maskini walioogopa kuiachia pesa yao mwanzoni, wakati huu uweza kuituma kwa matajiri hao na mzunguko uendelea hivyo hivyo na mwisho ni umaskini uliokithiri.



Kama tulivyoona kuwa kuna milango miwili ya pesa kuingia na kutoka. Mlango wa kwanza ni wa kuingilia (pesa inaingia mfukoni) na wa pili ni wa kutokea (pesa inatoka nje ya mfuko wako). Pesa ikishatoka nje ya mfuko wako, kuna mambo mawili ambayo yanatokea; kwanza pesa inaweza kutumwa mali ambayo iwapo itaongezewa thamani na kutoa bidhaa au huduma ambayo ikiuzwa tena inarudisha ile pesa iliyotoka mwanzoni na nyongeza juu (faida) na hii yongeza ni kwasababu ya thamani iliyoongezeka.  Pili pesa inaweza kutoka nje ili kufuata vitu ambavyo kwako wewe unakuwa ni mtumiaji wa mwisho; kiasi kwamba pesa iliyotumwa vitu vya aina hii, kamwe haiwezi kurudi hata ungefanyaje.



Watu wengi hasa waajiriwa pamoja na wakulima, huwa pesa zao zikishatoka kwa mwenyewe, mara nyingi huwa hazirudi kwasababu ya kutumwa vitu ambavyo wewe ndiye mtumiaji wa mwisho. Sababu kubwa ya waajiriwa ufanya hivyo ni kwasababu ya kutegemea mshahara mwisho wa mwezi. Hali hii humfanya mtumishi pamoja na mkulima kuishi maisha ya kawaida sana ambayo huwa hayabadiliki miaka nenda rudi. Baadhi ya vitu ambavyo pesa ikitumwa kuvifuata yenyewe hairudi ni vingi sana; mfano: Runinga Redio, Karo za wanafunzi, gari la kutembelea, n.k.


Bila kuingilia mipangilio mbalimbali ya watu walionayo, unaweza kuona kuwa pindi tu tunapoanza kazi ya kuajiriwa tunaanza vizuri lakini muda mfupi tu! tunawahi kutekwa na utamaduni wa kupeleka pesa kule ambako huwa hairudi. Na kwenye jamii tulizomo watu wanahamasishana kufanya hivyo. Na mpaka sasa watu wengi wamekuwa wakiishi kwa mazoea, kwamba unapopata ajira eti unashauriwa na wenzako kununua kiwanja na kujenga nyumba ya kuishi na vitu vingine vyenye kupeleka pesa bila kurudi.  

Watanzania, tunahitaji kubadili tabia pamoja na mtazamo wetu juu ya mapato na matumizi ya pesa; tunahitaji kujifunza ni jinsi ya kutuma pesa ikarudi pamoja na vitu. Pia, tunahitaji kuwa na mikakati na mbinu za namna ya kuifanya iwe nyingi badala ya utaratibu uliozoeleka wa kubana matumizi. Tukiweza kuyafanyia kazi yote haya hakika tutakuwa tumepiga hatua moja muhimu sana ya kutufikisha kwenye mafanikio tuyatakayo.
 
MWANZO WA KUIPATA PESA NI KUIJUA KWANZA!
Je? Na wewe ni mmojawapo wa wanaotafuta pesa? Kama jibu ni ndiyo, hiyo pesa unajua ni nini? mbali na kufahamu sura tu ya sarafu na noti? Ukiacha hilo, kuna cha zaidi unachojua kuhusu pesa? Ikiwa jibu ni “hapana” sasa wewe pesa utazipataje wakati huzijui? Mara nyingi watu husema kuwa, “huwezi kuona kitu usichokijua”! Mpaka sasa, ufahamu na uelewa uliopo juu ya pesa ni mdogo sana labda tu! ufahamu uliopo ni wa kujua jinsi pesa zinavyogawanyika na walio wengi tunafahamu zaidi kutoa na kujumlisha pesa, hasa wakati wa kurudisha chenji kwa mteja. Ukiacha hilo, taswira kubwa na ndefu iliyopo nyuma ya pesa (noti na sarafu) haionekani kirahisi kwa watu walio wengi. Ufahamu na uelewa mdogo juu ya maana pana ya pesa upo kwa watu wengi, na hali hii ni kwa wote waliokwenda shule na wale ambao hawakwenda kabisa.  

Ukweli ni kwamba “Pesa ni kitu chochote kinachowezesha watu kubadilishana vitu na huduma. Hapa ndo kuna mkanganyiko kwasababu watu wengi mpaka sasa wanaamini pesa ni kitu halisi na hivyo kusababisha wao kuweza kuiabudu na kuamini pesa kama inavyoonekana katika hali yake ya noti na sarafu. Mtazamo wa kuichukulia pesa kama kitu halisi, unawafanya walio wengi kuwekeza nguvu kubwa Katika kusaka/kutafuta pesa yenyewe kama ilivyo. Lakini wakisha ipata wanagundua kuwa, hitaji lao siyo makaratasi ya noti bali ni vitu na huduma mbalimbali hapo ndipo huzipeleka kwa wenye vitu na huduma, huku wakibakia tupu kabisa.

Katika kutafuta pesa kunakuwa na dhamira tofauti kati ya maskini na tajiri; “Watu maskini wanawekeza muda na nguvu yao kwa dhamira ya kutafuta pesa lakini watu matajiri wanawekeza muda, akili na nguvu yao kwa dhamira ya kutafuta “vitu na huduma”. Kwasababu maskini wengi waliamini kuwa mwisho wa utafutaji wao ni pesa, basi ndipo ugundua kuwa sio mwisho, kumbe mwisho wao ni kupata vitu na Huduma (chakula, dawa, mavazi; usafiri, elimu, utaalam, nguvukazi n.k.). Kwahiyo, pamoja na kutafuta pesa hiyo kwa kutumia nguvu kubwa na muda mrefu, mtu huyo ujikuta akilazimika kuzipeleka mwenyewe kwa tajiri ambaye wakati huo ana vitu na huduma fulani fulani. Kwa maana nyingine tunaweza kusema kuwa watu hawa wanaishi kwa kutafuta pesa na kisha kulipa bill! au madeni basi.

Mahitaji ya mwanadamu ni mengi sana na hayana kikomo, lakini pamoja na hayo, mahitaji haya yamegawanyika katika makundi makuu mawili: yaani “Vitu na Huduma”. Tunaposema “Vitu” inamaanisha vitu halisi na vinavyoshikika kama vile nguo, meza, komputa simenti, gari, simu, vyombo, spare, vitabu n.k); na tunaposema “Huduma” ni vitu ambavyo havishikiki navyo ni kama; usafiri, habari, utaalam, ulinzi na usalama, maombi, ufundi n.k. Kwahiyo, kutokana na ukweli huo hapo juu, ndiyo maana siku zote pesa itakwenda kule kulipo na vitu au huduma hakuna sehemu nyingine.

Kutokana na ukweli huu, ni wazi kwamba unapoona pesa imeingia mfukoni mwako, basi ujue kuna mtu ametuma pesa hiyo kufuata kitu fulani kwako, na iwapo huna kitu chochote ulichonacho basi hutapata pesa yoyote kwasababu hakuna kitu cha kufuata kwako. Sasa unachotakiwa kufanya leo ni kuanza kubadili swali ambalo watu wengi ujiuliza pindi wanapohitaji kupata pesa; swali lenyewe huwa ni hili hapa: “Nitapata pesa wapi?” na kwa kuwa wengi ujiuliza  swali hilo, ndiyo maana huishia tu! kutafuta pesa bila mafanikio.

 Iwapo utaendelea kujiuliza swali la nitapata pesa wapi ndivyo itakavyozidi kuwa vigumu kupata jibu ambalo litakuongoza kupata pesa. Kwahiyo, mtanzania mwenzangu ni wakati sasa wa kubadili swali lako kutoka “nitapata pesa wapi?” kwenda “Pesa itakuja kwangu kufuata nini?”. Na kila mara utakapojiuliza swali la pesa itafuata nini kwako, basi jibu jibu lake tu! litakuwa ndiyo pesa yenyewe kwa maana nyingine utaona watu wakibisha hodi mlangoni kwako, kwaajili ya  kukuletea pesa ambayo miaka yote umekuwa ukikimbia huku na huko kuitafuta bila mafanikio!. Sasa unachotakiwa kufanya ni utafiti katika mazingira yanayo kuzunguka na maeneo mengine unayoweza kuyafikia ili kutambua mahitaji, kero na changamoto zilizopo. Matokeo ya Utafiti yatakusaidia kubuni na kuzalisha vitu au huduma ili kukidhi mahitaji ya jamii husika, na ukifikia hapo ndipo utaona ndani muda mfupi watu wakituma pesa ili ikafuate vitu na huduma kutoka kwako.

Kwahiyo, uwanja ni wako wewe mtanzania unayetafuta mafanikio, kwani tuna imani kubwa sana kuwa unaweza kupata pesa nyingi, iwapo utakubatia na kuifanyia kazi falsafa hii ya “Pesa itakuja kwangu kufuata nini?”.


SIRI YA WALIOFANIKIWA NI KUWEKEZA KWAO ZAIDI KWENYE AINA YA MAPATO YASIYOKUWA NA KIKOMO (TULI)
Unapoanza safari yako kuelekea kwenye mafanikio makubwa ni vizuri ukafahamu ni aina gani ya kipato unachopata kwa sasa? Kwahiyo, ili kuweza kufahamu sifa na aina za vipato, ni muhimu kujua kuwa zipo aina kuu tatu za vipato ambazo ni: Mapato ya Ajira (mshahara); Mapato Hai (kujiajiri); Mapato yasiyo na kikomo au Tuli, (Passive Income).
1.      Mapato ya Ajira (Earned Income)
Haya ni mapato yanayotokana na kufanya kazi ya kuajiriwa (mshahara), ambayo mtu huyapata kutokana na ajira yake. Katika aina hii ya kipato, vigezo vya kukuwezesha ulipwe ni pamoja na aina ya kazi na wadhifa au cheo chako. Pia, mapato haya yanajumuisha mapato yoyote yatokanayo na ajira binafsi (kujiajiri), biashara ndogondogo na shughuli nyinginezo ambazo unapata kipato kutokana na juhudi na muda uliotumika. Kwa maana nyingine, ni kwamba kama husiposhugulika au ukasimama kufanya kazi na kipato kinakoma pale pale.
Ø  Uzuri wa Mapato ya Ajira
·        Mapato yanaongezeka zaidi kulingana na muda na ukubwa wa shughuli inayofanya
·        Hauitaji mtaji kuweza kupata mapato haya
·        Mtaji ni nguvu au ujuzi wako mwenyewe
Ø  Ubaya wa Mapato ya Ajira
·        Uwezi kupata utajiri wa kudumu kwa aina hii ya mapato yanayotokana na mshahara. Kwasababu mshahara unapata, unakula na unanaisha.......Unapata unakula zinaisha.....
·        Siyo mapato endelevu, ukiacha kufanya kazi mapato yanakoma.
·        Mapato haya ya ajira yanatozwa kodi kubwa kuliko aina nyingine zote za mapato na Waajiriwa wanalijua vizuri hili.
Mfano; kwa mtu anayelipwa mshahara wa kiasi cha 1,350,000/- anakatwa kodi hivi:
Aina ya Makato
Kiasi (TSh)/Mwezi
Kodi (Income Tax)
260,400.00
Bima ya Afya
40,500.00
Chama cha Wafanyakazi
27,000.00
Mfuko wa Pensheni
67,500.00
Jumla
394,900.00
Sasa, ebu fikiria mtu anakatwa karibu Shilingi 400,000/- kila mwezi, kiasi ambacho kwa mwaka kinafikia karibu shilling 4,800,000/-. Unaweza kukuta mtu ana biashara yenye mtaji upatao shilingi million 15, siajabu kukuta analipa kodi kiasi kisichozidi shilingi 500,000/- kwa mwaka.
2.      Mapato Hai (Active Income)
Aina hii ya mapato, kwa kiasi fulani inafanana na mapato ya ajira yanayo jumuisha mishahara, kwani mapato haya yanatokana na kuuza na kununua bidhaa kubwa kubwa kama magari, nyumba, kiwanja n.k. Mchakato huu ni kwamba, unanunua kitu halafu unakiuza kwa faida, halafu basi. Ili uweze kupata mapato mengine inakubidi, utafute kitu kingine au ununue kitu kingine haraka ndipo upate tena pesa. Maana yake ni kwamba lazima uwe kazini (active) muda wote huku ukiendelea kuchakarika ndipo upate mapato. Kama ilivyo kwa mapato ya mshahara, pindi unapoacha kununua na kuuza vitu, mapato nayo yanakoma mara moja.
Ø  Uzuri wa Mapato Hai
·        Mapato haya hayahitaji watendaji kazi wengi ili kufanikisha shughuli ni wewe tu mwenyewe.  
·        Kodi yake ni ndogo kulinganisha na ile ya mapato ya ajira
·        Unapata zaidi kutokana na jitihada zako za kutafuta na uchangamkia fursa.
·        Unaweza kufanya na kupata pesa hata pasipokuwa na mtaji. Mfano, unachukua mali (sema gari), Unamwambia jamaa utamletea pesa yake baada ya siku mbili hivi, kumbe wakati huo umeisha tafuta mteja tayari unampelekea, unauza unamlipa jamaa wewe unabaki na faida. Tayari umeisha tengeneza pesa bila hata kuwa na mtaji ~ yaani ni ujanja ujanja tu!
Ø  Ubaya Wake
·        Inahitaji utaalam na ujanja wa hali ya juu na kufahamika pia, unaweza kupewa vitu feki, kuzurumiwa, kuibiwa, kupata hasara n.k.
·        Unaendelea kushughulika wewe mwenyewe ndipo unapata faida
·        Unaweza kupata hasara kutokana na kubadilika kwa hali ya mambo juu ya bidhaa husika. Mfano: mitindo/fasheni, msimu, bei n.k.
3.      Mapato Yasiyo na Kikomo (residual or passive income).
Ni mapato mtu anayoyapata pasipokuwa na ulazima wa kushughulika/kufanya kazi kwa wakati huo au kwa maana nyingine ni mapato “Tuli”. Mapato haya mara nyingi yanatokana na kazi au shughuli uliyokwisha kufanya kitambo na kuendelea kupata mapato haya “Kimya Kimya”. Unayapata kutokana na vitega uchumi ulivyoweka. Mfano: kama umenunua nyumba na kupangisha na kila mwisho wa mwezi unapewa kodi ya pango, basi mapato hayo ndiyo yanaitwa yasiyo na kikomo au TULI.
Unashughulika mara moja tu na kisha unaendelea kupata pesa kwa muda mrefu bila hata wewe mwenyewe kushughulika tena/ zaidi. Pia mapato yatokanayo na Mtandao,  nakala za albamu ya muziki, filamu au vitabu n.k. ni hayana kikomo. Unaendelea kutoa nakala na kuuza miaka na miaka.
Ø  Uzuri MapatoYyasiyo na Kikomo (Tuli).
·        Unaendelea kupata pesa kwa muda mrefu baada ya kazi/shughuli ya awali
·         Unakuwa na MUDA  wa ziada kufanya mambo mengine. Unabaki  kucheza gofu na kutalii huku pesa zinaingia
·        Hayatozwi kodi kubwa kama mapato ya aina nyingine.
Ø  Ubaya MapatoYyasiyo na Kikomo (Tuli)
·        Wakati mwingine hugharimu sana kuwekeza katika hatua ya awali.
·        Huitaji uvumilivu (patience) kwani yaweza kuchukua muda mrefu kabla ya kuanza kupata mapato haya. “Lakini Yakianza Kuingia Unatumia Hadi Unasahau”.
Hizi ndizo aina kuu tatu za mapato yatokanayo na shughuli mbalimbali katika maeneo makuu manne ya mafanikio ya kifedha - Biashara, sanaa, michezo, uvumbuzi wa kisayansi au teknolojia, utunzi wa vitabu pamoja na kujenga mtandao (Network Marketing Business). Kwahiyo, kama una ndoto ya kupata mafanikio makubwa kimaisha, unashauriwa kufanya shughuli zinazopelekea kupata mapato “Tuli”.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba mapato Tuli, ndiyo mapato pekee ambayo ni imara, endelevu na yanarithika. Sababu nyingine inayotufanya tukushauri kupata mapato haya ni kwamba, watu wengi waliofanikiwa (matajiri) duniani, wamejipanga na kujikita katika kupata mapato haya. Ili kuendelea kujielimisha zaidi juu ya undani wa mapato haya - "tuli", kupitia mtandao wako wa maarifashop, tutaendelea kukuletea mafunzo juu ya aina hii ya mapato, ili hatimaye kila mmoja wetu aweze kuchukua hatua za maksudi tayari kuelekea kwenye maisha ya ndoto zetu.
~TWENDE KAZI PAMOJA~!


JE? UTAMTABUAJE RAFIKI YAKO MWENYE IMANI SAHIHI JUU YA PESA?

Wakati fulani ndani ya mwezi mwaka huu, nikiwa kwa mtoa huduma ya kubrashi viatu, nilikutana na jamaa mmoja akiwa akiongelea juu ya mambo ya maisha na mtoa Huduma huyo. Nilipofika waliendelea na stori zao na mimi mara moja moja nikawa naruhusiwa kuchangia hoja iliyokuwa mezani. Wakati huo wote walijadili sana juu ya changamoto za kimaisha, ikwemo tatizo sugu la ukosefu wa pesa na hivyo kufanya maisha kuwa magumu sana. Mimi pamoja ya kwamba nilichangia lakini nilikwa nasikiliza zaidi mjadala ulivyokuwa ukienda ili niweze kujifunza kitu. Baada ya mazungumzo hayo nilipata wazo la kutafakari na kuanza kuandika makala juu ya “Imani Yako Kuhusu Pesa!” wazo hili lilitokana na ukweli kwamba watu wawili hawa walihitimisha mjadala kwa kusema kuwa “Fedha ina Siri Kubwa” wakiamanisha kwamba kanuni au njia ya kupata pesa haijulikani. Ukienda mbele Zaidi unagundua kwamba, tayari kwenye jamii kumekwisha jengeka imani kwamba kupata pesa ni kubahatisha, Kiasi kwamba wengi wao wanaotafuta pesa hawana uhakika kama ipo siku watapata.

Kutokana na hitimisho hilo la kwamba “pesa ina siri kubwa” niwazi kuwa kuna ombwe la uelewa na ufahamu kuhusu maana halisi ya pesa. Na niseme kuwa imani iliyopo kwa sasa juu ya pesa yawezekana siyo sahihi (ni potofu). Upotofu huu wa imani juu ya pesa  unajidhihirisha Katika matukio mengi hapa nchini kwetu Tanzania na nchi za jirani, ambapo kumekuwepo na matukio mengi ya watu kujaribu kutumia ushirikina ili kupata mafanikio ya haraka na hasa mafanikio ya kifedha.

Kama ilivyo imani Katika dini kwamba mwanadamu aweza kuwa na imani potofu juu ya wokovu au akawa na imani iliyo ya kweli kuhusu wokovu na linapokuja swala la upatikanaji wa pesa ni hivyo hivyo, kwani imani yetu tuliyonayo juu ya pesa imetokana kiwango cha uelewa tulionao. Lakini niseme kuwa ni bahati mbaya sana kwamba uelewa wetu juu ya kitu pesa bado ni mdogo sana, licha ya kuwa “Pesa” ni moja kati ya vitu vichache vinavyopendwa sana duniani. Kama ilivyo katika dini zetu, kwa waumini wa madhebu yote, ili waweze kuwa na imani sahihi juu ya muumba wao, wanahitaji kwanza neema ya Mungu, lakini pia wanahitaji watu ambao wako tayari kujitoa na kufanya kazi ya Mungu ili kusaka ukweli na kuupeleka ukweli huo kwa watu wote kwa jina la “Habari njema” Hivyo basi kadili watu wanavyozidi kupata ukweli kuhusu wokovu ndivyo watazidi kujenga imani ya kweli au sahihi juu ya wokovu au kazi ya Mungu.

Kwahiyo, kutokana na mantiki hii ya wokovu, Ndiyo maana wengine tayari tumeanza kuchukua hatua ya kusaka ukweli juu ya “Fedha” ili ukweli huu uweze kusambaa kwa watu wote. Imani yangu ni kwamba, iwapo watu watapata ukweli huu kupitia makala hii au njia nyinginezo, basi ukweli huu, utawezesha wengi kubadili na kujenga imani iliyo sahihi. Kadili watu watakavyozidi kujenga imani sahihi juu ya pesa ndivyo itakavyokuwa rahisi kupata pesa na hivyo kuweza Kuboresha na kuishi maisha ya ndoto zetu.

Katika kutambua nani mwenye imani sahihi juu ya pesa, unaweza kuangalia dhana, misemo, methali na nahau juu ya pesa kwa mtu binafsi au kundi la jamii husika. Hivi vyote, ndivyo vigezo au viashiria tunavyoweza kuvitumia kupima imani ya mtu aliyonayo juu pesa. Kwa kufahamu imani yake iko wapi ni rahisi sana kufahamu iwapo huyo mtu ana imani sahihi au imani potofu. Mfano wa baadhi ya viashiria vya imani ya mtu juu ya pesa ni hivi hapa; ”Pesa ni Sabuni ya Roho” : Dhana hii ya kuamini kuwa pesa ni sabuni ya roho, inatuonyesha kuwa ndani ya fikra zetu tunadhani pesa ndilo hitimisho la kazi tuliyokuwa tukifanya bila kujali tumeifanya na kuumia kwa muda gani. Ukitaka kufahamu nani anaichukulia pesa kama hitimisho, utamuona tu anavyokuwa amechangamka na kuanza hata kubadili mfumo wa maisha ikibidi hata vyakula, vinywaji, mavazi, hubadilika kwasababu mtu huyu anajiona amefika mwisho na roho yake imesafishika. Kama alikuwa akifuga ng’ombe, sasa ataanza kutokuwajali na baadae mradi utakufa na mwisho zile pesa ambazo alikuwa ameishaanza kusahau zilikotoka na zenyewe zitaisha. Iwapo hii ndiyo imani yetu juu ya pesa basi ni wazi kwamba pesa hapa tunaichukulia na kuitumia kama mapato. Tatizo la kuiona pesa kama mapato huwezi tena kwenda hatua zinazofuata ili kukamilisha malengo yako ya kimaisha na badala yake unaishia njiani kabla ya kufika mwisho. Wale waliofanikiwa au wale matajiri, wakipata pesa bado haichukulii kama mapato badala yake utumia hiyo pesa kuanzisha mradi mwingine, na pesa yote inayopatikana Ndiyo utumika tena kuazisha mradi mkubwa zaidi ambao faida yake Ndiyo mtu kuitumia kwenye vitu vya hanasa (luxuries).

Kwahiyo, hili tuweze kuiishi imani hii ya “Pesa ni Sabuni ya Roho” ni lazima kufahamu kuwa ukishapata pesa unafurahi sana, lakini ni vizuri furaha hiyo isitusahaulishe tunako kwenda na tuendelee kuiona kuwa ni makaratasi ambayo tunahitaji kuyatuma kwa wengine ili tupate pesa nyingi zaidi kwaajiri ya kuwekeza kwenye kuzalisha vitu na huduma bila kikomo.

“Kupata pesa ni bahati, na kama ukuandikiwa na Mungu kuzipata hata ungefanyaje! Utapata” Usemi huu unaonyesha kuwa kana kwamba kuna baadhi ya watu ambao wamezaliwa na bahati ya kupata pesa na inaonekana ni wachache sana ukilinganisha na wale wasiokuwa na bahati. Kuendelea kuwa na imani hii vichwani ni janga la kitaifa kwasababu, kila utakapo anza mchakato wa kutafuta pesa fedha na ukakumbana na vikwazo na changamoto mbalimabli ni dhahili utakuwa wa kwanza kukata tamaa na kuingia kwenye mtego wa kutafuta njia za mkato ili kupata pesa.

Hili usiendelee kuamini kuwa kupata pesa ni bahati, ni vizuri ukafahamu kwamba kila mtu amezaliwa na uwezo wa kupata pesa haitakayo. Kinachohitajika kabla ya kutafuta pesa ni kuchukua muda wako ukafikiri na kutafakari majibu ya maswali haya; Je? Pesa ni kitu gani?, Pesa hupatikana wapi?, kwanini wengine kipindi Fulani pesa na baadae kuishiwa?; Je? Pesa inakujaje kwako na inapoteaje? Je? Wewe unatafuta shilingi ngapi mwaka huu? Kwako fedha itafuata nini? n.k. Kadili utakavyoweza kujibu maswali haya wewe mwenyewe itakufanya utafakari kwa kina na majibu utakayopata yatakufanya ubadili imani potofu uliyokuwanayo na baadae kujenga imani mpya kuwa “Kupata pesa ni Kuwa na Kitu au Huduma ambayo itawafanya watu wengine waitume pesa yao kwako kufuata vitu ulivyonavyo pamoja na huduma huliyonayo. Na hili uweze kupata vitu na huduma msingi wake ni kazi na ubunifu, iwapo utavitumia hivi vipaji yaani “Kazi na Ubunifu” sioni sababu nyingine ya kukufanya ukose pesa.

Ewe mtanzania chunguza imani yako juu ya pesa, ili ujitenge na wale wanaotumia njia ya mkato na kutafuta utajiri wa haraka. Kama ukikuta imani yako ni potofu, basi kata shauri leo na kubadili ili uwe na imani sahihi juu ya pesa kabla ya kuanza kuitafuta.
~KARIBU TWENDE KAZI PAMOJA~

1 comment:

Unknown said...


TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15,000 Hadi $ 72,000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
SAA ZA MAFANIKIO YA Ufanisi wa Huduma na Viwango vya Riba 2% KWA WAFANYABIASHARA
NA BINAFSI
MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
philipmorganloanservice00@gmail.com

JAZA NA URUDI

Jina:
Kiasi cha mkopo:
Muda:
Jinsia:
Nchi:
Lengo:
Nambari ya simu ya rununu:

JIBU LAKO LINAHITAJIKA MARA MOJA