Monday, July 31, 2017

Muuzaji na Mnunuzi Nani ni Mfanyabiashara?


Katika maisha yetu ya kila siku hapa duniani, kuna watu wanaofikiri na kuamini “sisi siyo wafanyabiashara wao ni wafanyabiashara”. Wengi wanaamini kuna kundi fulani la wafanyabiashara. Kutokana na mtazamo huu juu ya biashara, wengi wanajiaminisha kuwa wanaweza kuishi maisha mazuri bila kuwa wafanyabiashara. 

Watu wengi wanadahani mfanyabiashara ni

Monday, July 24, 2017

Hatari ya Kushindwa Kupanga ni Kama Hii



Nikiwa mmojawapo wa washiriki wa kikao cha kamati ya mradi wa kilimo siku ya tarehe 13/07/2017, mwenyekiti wa kamati alifungua kikao na kukumbusha wajumbe kuwa mojawapo ya majukumu ya kamati ni pamoja na kupanga namna bora ya uendeshaji wa shughuli za mradi. 

Katika kusisitiza hilo alisema “kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa”. Maneno haya yalinigusa sana na yalinifanya kutafakari zaidi juu ya maana ya maneno haya katika maisha yetu ya kila siku.

Katika maisha kuna vitu ambavyo vipo na havitegemei uwepo wako. Vitu ambavyo havitegemei uwepo wako ni

Monday, July 10, 2017

Dawa ya Ujasiri wa Kukopa Pesa Benki Inapatikana Hapa



Kila ukigusia suala zima la watu kukopa pesa, wengi uonyesha wasiwasi wao mkubwa juu ya kitu mkopo. Kutokana na mtazamo uliopo juu ya mkopo, inaonekana kuwa mkopo ni kitu cha mwisho mtu kuweza kukifanya hasa hapa Tanzania. Ukweli ni kwamba jamii yetu imejaa woga juu ya mikopo hasa ile itolewayo na benki za biashara. Niseme kama wewe ni mjasiriamali wa kweli, uhitaji kuwa mwoga, bali