AfyaYetu


HUU NDIO MUUJIZA WA VYAKULA VINAVYOISHI
  
“Siri ya kufanya kazikwa bidii bila kuchoka ni kula vyakula vinavyoishi”~ Cypridion Mushongi


Wewe kama binadamu anayejitambua na kujipenda, unahitaji kufahamu kuwa wewe ni matokeo ya kile ulacho kila siku. Kwa kufanya mageuzi katika lishe yako, unaweza kabisa kubadili maisha yako kuanzia muonekano, nishati/nguvu ya mwili hadi uchumi. Wengi wetu tayari tunafahamu juu ya ulaji wa kunenepesha mwili au kupunguza mwili, lakini ni watu wachache sana ambao wanatambua jinsi ya..
kutumia chakula katika kufungua nguvu ambayo mara nyingi upotea kutokana na kutumika katika kusaga na kulainisha baadhi ya vyakula ambavyo havisagiki haraka mfano nyama n.k.



Mikakati yote ya kukuza uchumi, kuleta utulivu wa akili na mbinu binafsi za ustadi wa maisha hazitakusaidia kama hautakuwa na nguvu na afya ya kufanya yote yale yanayohitajika ili kufikia maisha ya ndoto yako. Makala hii ni juu ya muujiza wa chakula ambacho uwekwa mwilini mwako. Kwa kujali zaidi kupitia lishe sahihi, unapata uhakika wa kuishi maisha marefu na uwezo wa kufikia ndoto zako za maisha bora. Kwa kuliacha suala nyeti la chakula na lishe lijiendee vyovyote, ni wazi kwamba ndoto zako nyingi zitavunjikavunjika na kamwe hutaweza kuzitimiza hata siku moja.



Katika nchi ya India ya kale, watu wake waliamini kuwa akili na ubongo imara ni vitu vilivyo na uhusiano wa moja kwa moja na aina ya chakula na lishe ya mtu husika. Vyakula vyepesi na ambavyo siyo vya asili ya nyama kama vile mbogamboga na matunda, walivipendelea zaidi. Watu hawa wenye asili ya India na Asia, walikuwa wakiamini kuwa kutiririka kwa nguvu binafsi na nishati mwilini ni kitu kilichokwamishwa zaidi na ulaji wa nyama. Utafiti wa kisayansi wa hivi karibuni umedhihirisha kuwa utendaji kazi hafifu wa mtu unahusishwa moja kwa moja na hali yake ya akili na mwili. Wito kwako msomaji ni kwamba ni muhimu ukahakikisha unajali sana hali ya akili na mwili wako na kwa kufanya hivyo utatengeneza maisha mazuri unayostahili.



Ulaji vyakula vinavyoishi: Hatua kubwa kupata afya na mwili imara!

Watu wa kale kutoka jamii ya “yogis” huko milima ya “Himalayas” ni watu wanaotoa somo zuri sana juu ya suala zima la kuishi maisha marefu, nishati/nguvu ya mwili na uimara wa mwili na akili. Wengi wao tunaambiwa ni watu wanaoweza kuishi maisha ya zaidi ya miaka 100 na kudumisha uwembamba na miili imara yenye nguvu sana maisha yao yote, na kuweza kufanya shughuli nzito zinazohitaji ujasiri mkubwa vizuri kwa kile wamarekani wanachoita miaka ya mwisho. Watu hawa wanaweza kukaa hadi zaidi ya wiki moja bila kula chakula na bila usingizi. Pia, ni watu wenyekuwa na uvumilivu wa kipekee ambao wanaweza kuvumilia maumivu makali sana. Ni siri gani iliyopo juu ya maisha marefu na ya ujana kwa watu hawa? Jibu ni rahisi kwamba, huwa wanajitahidi kula chakula kiasi na wanafuata utaratibu wa kula vyakula vinavyoishi au hai na vya asili.



Kwa taarifa ni kwamba vyakula vinavyoishi ni vile ambavyo vimekuwepo au vimetokana na njia ya asili ambayo ni muunganiko wa nishati ya jua, hewa, udongo na maji. Lishe yenye vyakula vya namna hii, inasisitiza matunda (na juisi zake), mbogamboga na nafaka. Kwa kuweza kufanya mabadiliko na kuhakikisha asilimia 70 ya lishe yako inakuwa ni matunda, mbogamboga na nafaka, utakuwa umepiga hatua ya kwanza kuelekea uimara wa mwili na maisha yenye hamasa kubwa.

Hapa ni baadhi tu ya faida zilizothibitika ambazo utazipata endapo utaanza kutumia vyakula vinavyoishi ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango kikubwa cha nguvu zako na stamina; kuongezeka kwa utulivu wa akili na ubunifu; kupungua kwa kitambi na mafuta mwilini; kulainika kwa ngozi; kupungua kwa mahitaji ya usingizi, chakula kusagika kwa urahisi; kuongezeka kwa uchangamfu wa akili; kuwa na kumbukumbu nzuri; maisha marefu na athari kidogo za magonjwa; kuwa na hali ya kujisikia utulivu utokanao na kuwa na hali nzuri kiafya kwa ujumla.



Lishe ambayo imesheheni mbogamboga, nafaka na matunda, ndio hasa asili yetu ililenga kutupatia sisi binadamu. Kwa mfano, meno yetu na utumbo wetu unatofautiana sana na ule wa wanyama wanaokula nyama kama mbwa, LAKINI meno yetu yanafanana na wanyama wanaokula matunda. Kutoka kwenye nyama kama vile ya ngombe, mbuzi, kuku n.k utupatia lishe ambayo ni ya daraja la pili kwa umuhimu mwilini. Nyama inakuwa kwenye daraja la pili kwasababu inapatikana kwa myama anayekula nyasi, mbogamboga na matunda ya asili.



Kimsingi bidhaa kama nyama imeonekana kuwa na matokeo hasi mwilini na pia inakosa kiasi kikubwa cha vitamini na madini muhimu katika ustawishaji wa mwili wa binadamu. Madini na vitamini ni viasili ambavyo vinahitajika mwilini ili huweze kufanyakazi vizuri na kwa ufanisi mkubwa. Jambo lingine muhimu kulifahamu ni kwamba, nyama ni chakula kigumu kusagika tumboni, na kwa maana hiyo ni chakula kinachosagwa kwa kuhitaji kiwango kikubwa cha nishati. Matokeo yake, kusagwa kwake kunamaliza kabisa ile nishati/nguvu yote iliyohifadhiwa mwilini na ambayo kama isingepotea kusaga nyama, ingeweza kutumika kufanya kazi nyingine za uzalishaji mali. Ebu jaribu kulinganisha jinsi ujisikiavyo mara baada ya kula nyama steki, na mara baada ya kula mbogamboga na matunda au saladi?



Vyakula vya asili kama vile matunda vinasagika kwa urahisi sana tumboni na vinatumia nishati kidogo sana. Maana yake ni kwamba, ulaji wa vyakula hivi unauachia mwili kiasi kikubwa cha nishati ambayo inakuwepo kwaajili ya kufanya shughuli nyingine muhimu, hasa zile za uzalishaji na shughuli nyinginezo za kutimiza ndoto zako. Siri mojawapo ya kufanya kazi kwa bidii na bila kuchoka ni uwepo wa hifadhi kubwa ya nishati mwilini. Unaweza ukawa unawahi shambani, ofisini, na mahala pengine, lakini kama huna hifadhi ya nishati ya kutosha mwilini ni kazi bure. Maana utakuwa unachoka haraka kila unapoanza kazi za siku husika. Kwa wale tunaofanya kazi maofisini ni mashahidi wa sisi wenyewe au marafiki zetu wanaosinzia ofisini na kwenye vikao – tatizo hili linasababishwa na uhaba wa nishati mwilini ambayo kila mara inatumika zaidi kusaga vyakula kama nyama n.k. 



Kama nyama ni kitu kibaya kwetu, kwanini tunaila?

Watetezi wengi wa ulaji wa nyama wanadai kwamba, ulaji wa mbogamboga hautoi protini inayotakiwa mwilini. Lakini, hiyo tunaweza kusema kuwa ni kejeli kwasababu, wale walao nyama siku zote upata protini isiyokuwa bora kwa binadamu. Ukweli ni kwamba protini ya kutoka kwenye nyama ina tindikali (acid) hatari mwilini aina ya “Uric acid” ambayo lazima ivunjwevunjwe na ini jambo ambalo linaweza kuleta athari za kiafya siku za mbeleni.



Mbogamboga na matunda pamoja na bidhaa zingine za wanyama kama vile; maziwa ni chanzo cha protini yenye ubora wa hali ya juu (daraja la kwanza) kuliko ile itokanayo na bidhaa za nyama. Ushahidi uliopo ni kwamba unahitaji kuangalia mnyama mwenye nguvu nyingi duniani. Tembo, Faru, Nyani – (wanayama hawa wananguvu mara 30 zaidi ya binadamu), na wote wanaweza kuishi kwa kutegemea majani, mbogamboga, na matunda. Matunda na mbogamboga vitakupatia protini unayohitaji ambayo ni ya daraja la kwanza.



Sehemu kubwa ya makala hii imetokana na maudhui ya kitabu cha Bw. Robin S. Sharma ambacho kinajulikana kama MEGALIVING! 3O DAYS TO A PERFECT LIFE: The Ultimate Action Plan for Total Mastery of Your Mind, Body & Character. Kama unapenda kupata nakala tete (soft copy) ya kitabu hiki bonyeza neno KITABU; na kisha weka barua pepe yako, nitakutumia kitabu hicho ndani ya masaa 48. Kama uliwahi kusajiri barua pepe yako hapa MAARIFA SHOP; basi wewe nitumie tu majina yako kwa whatsap no: 0788 855 409.

Endelea kunufahika na http://maarifashop.blogspot mpaka utakapohisi umefanikiwa bila kikomo.


 



BILA "MABORESHO" IMANI YAKO INAWEZA KUKUANGUSHA

  • Kila binadamu anapendelea kufanya kitu kadiri anvyotumwa na imani yake
  •  Imani Mbaya = Matokeo Mabaya
Uzoefu katika maisha ya binadamu umeonyesha kuwa kile unachoamini zaidi ndicho ukuletea mafanikio uliyonayo. Siku za nyuma kidogo nilichukua likizo yangu ya mwaka, wakati nikiwa likizo nilibahatika kwenda Entebbe Uganda, nikiwa huko nilitembelea hoteli ya Imperial Botanical Beach, lengo langu lilikuwa ni kuamsha upya mwili na fikra zangu ndiyo maana niliweka jitihada za kuuzuria mafunzo ya jinsi ya kujenga na kutunza afya ya mwili. Hakika nilipata nilipata somo la thamani kubwa kwa maisha yangu yote.

Kila binadamu anapendelea kufanya kitu kadiri anvyotumwa na imani yake: Siku ya kwanza nilipokutana na mtaalamu wa mazoezi ya viungo na afya, aliniuliza kuhusu tabia na utaratibu wangu kwa ujumla juu ya ulaji wangu wa chakula kwa siku. Nilimwambia kuwa, mara nyingi huwa ninakula milo miwili kwa siku; yaani kifungua kinywa na au chakula cha mchana na usiku. Wakati nikimueleza hayo nilifanya hivyo huku nikiangalia saa yangu ya mkononi, ndipo nikashitukia ni saa kumi na mbili jioni na baadae kugundua kuwa sijala chochote kwa siku nzima. LAKINI bado nilijisemea kimoyomoyo “Kwangu mimi kula siyo kipaumbele ”.

Baada ya mtaalamu kusikia kuwa huwa na kula mara mbili kwa siku aliniangalia na kuonyesha kusikitika kidogo, lakini aliendelea kusema, “Unatakiwa kula milo mitatu kwa siku.”
Kusikia hivyo nilimjibu kwamba, habari hiyo ya milo mitatu kwa siku nilikwishaiskia kabla. Lakini pamoja na kusikia habali hiyo, mimi imani yangu ni kwamba, iwapo nitakula milo mitatu kila siku, unene wangu utaongezeka sana. 

Mtaalamu wangu alicheka, na akazidi kusisitiza kuwa ninatakiwa kula zaidi wakati wa mchana kwasababu mwili unakuwa unafanya kazi sana. Kwahiyo, miili yetu uhitaji chakula cha kutosha nyakati za asubuhi, na mapema kabla ya saa za mchana (adhuhuri), na pia tunahitaji chakula kidogo nyakati za usiku, kwani muda wa usiku mwili unakuwa na kazi kidogo sana kwa maana nyingine unakuwa umepumzika.
Niliambiwa kwamba kwa mtu ambaye bado yuko vizuri kiafya, asipokula chakula cha kutosha ni kwamba badala ya mwili kuunguza mafuta, mwili utaunguza misuli na ikitokea hali hii basi ujue hutakaa huwe na kiwango cha uimara wa mwili unaoutaka.

Mimi nilikuwa ninaendelea kupigana na imani yangu iliyozidikuniambia kuwa, milo mitatu kwa siku itaongeza kilo moja ya uzito. Lakini kwakuwa nilienda kwa mtaalamu kwaajiri ya afya yangu, nilijifikiria na kuamua kufuata ushauri niliopewa na mtaalamu.
Wasikilize wataalamu: Kwa muda wa siku sita, nilianza kufanyia kazi imani mpya na kuanzia siku ya kwanza nikaanza kupata milo mitatu kwa siku. Niliamua kufuata masharti kama nilivyoelekezwa na mtaalamu kwa kuanza kula milo mitatu kwa siku. Kitu kimoja kilichojitokeza ni kwamba nguvu ya mwili iliimarika zaidi. Kuanzia nyakati za asubuhi, nilijisikia mwenye nguvu ya kutosha siku nzima. Niliendelea na mpango huu mpaka mwisho wa siku ya sita, siyo tu kwamba sikuongezeka uzito, bali badala yake nilipugua kilo kadhaa.
Kitendo cha kuamua kuachana na imani yangu juu ya idadi ya milo kwa siku, na kuamua kumsikiliza mtaalamu, kilinisaidia sana kufikia malengo yangu ambayo nisingeyatimiza hata siku moja kama ningeendelea kufanya yale niliyoamini miaka yote.

Imani mbaya = matokeo mabaya: Hoja muhimu juu ya stori hii ni kwamba, nilikuwa na imani potofu ambayo ilijengeka siku nyingi na imani hii kimsingi ilinizuia kusonga mbele na hatimaye kushindwa kutimiza malengo yangu ya kiafya. Pamoja na kwamba nimesikia tangu nikiwa mdogo, kwamba mtu mzima anatakiwa kupata milo mitatu kwa siku, sikuwahi kuamini kama faida zitokanazo na kula milo mitatu kwa siku zilikuwa za kweli. Nilikuwa na taarifa, lakini, faida hizi sikuzipata mpaka pale nilipoamua kufunguka na kuamua kujaribu yale niliyoelekezwa na mtaalamu —ndipo nilipopata uzoefu na elimu ya kweli juu ya kile kilichoonekana kufanya vizuri kwangu.

Kwa vyovyote vile, ukweli huu ni rahisi na unaweza kutumika kwenye hali yoyote katika maisha. Sasa swali kwako, “ni imani zipi zinazokurudisha nyuma kiasi cha kushindwa kufikia mafanikio ya kipesa au ndoto zako? Na utafanya nini kuondoa imani hizo?

Iwapo utapenda kujifunza jinsi ya kutambua na kuondokana na imani ambazo siku zote zimekurudisha nyuma pale ulipojaribu kutafuta uhuru wa kipato na mafanikio kimaisha, bonyeza; http://eepurl.com/bkXr3r kuweka barua pepe yako, ili kujiunga na programu ya mafunzo juu ya mafanikio ya kifedha.

Mafunzo haya yatatolewa bure kupitia barua pepe utakayosajiri hapa: http://eepurl.com/bkXr3r

Mafunzo yataanza tarehe 15/Septemba/2015 hadi 30/Septemba/2015.  Kwa kujiunga na mafunzo haya utapata thamani kubwa sana, ikiwa ni pamoja na kubadili mitazamo hasi uliyonayo juu ya kupata pesa. Pia utapata kujua mbinu na njia za uhakika utakazozitumia kufikia maisha ya ndoto yako kwa uhakika na kwa muda mfupi zaidi. Kama unafikiri program yetu haikufai huko sahihi; LAKINI bado ninakushauri ujitahidi kutafuta mtu, ambaye atakufundisha na kukupa mwongozo wa jinsi ya kufikia uhuru wa kipato. 

Kwa maelezo zaidi juu ya prograu hii ya mafunzo whatsApp: +255 788 855 49 au E-mail: mchumieconomist2009@gmail.com.
KARIBU TWENDE KAZI PAMOJA



CHIMBUKO LA PESA NI HILI HAPA

  •  Afya Bora Ndiyo Machimbo ya Kudumu  ya “Pesa” tuliyonayo!
  • Watu Wengi  Bado Wanaamini Kuwa Kitu Kinachoitwa “Afya” Kitajileta Chenyewe!
Katika maisha ya siku hizi inashangaza sana kuona kuwa pesa tunazotafuta zimekuwa zimekuwa adui yetu mkubwa wa miili na afya yetu kwa ujumla. Ndiyo maana leo hii, watu wengi “wanakula dawa kama chakula badala ya kula chakula kama dawa”. Maana yake ni kwamba, watu wengi wanayo pesa lakini, Asilimia kubwa inatumika kununua dawa ili waweze kusogeza maisha yao mbele. Mwanaharakati mmoja kutoka bara la Asia aliyejulikana kwa jina la “Dalai Lama”, alipoulizwa kitu ambacho kiliwahi kumshangaza zaidi kuhusu ubinadamu, alijibu kuwa ni Binadamu:

“Kwasababu, binadamu anatoa afya yake sadaka, ili kutafuta pesa. Alafu anatoa pesa yake sadaka, ili kurudisha afya yake. Na sasa anaanza kuhofia juu ya mstakabari wa maisha yake ya baadae (future), kiasi kwamba anashindwa kufurahia maisha yaliyopo wakati huu; Matokeo yake ni kwamba mtu huyu hawezi kuishi wakati huu (uliopo) au ujao; anaishi kama vile hatakaa aje kufa na alafu anakufa kama vile hakuwahi kuishi”

Maono ya mwanaharakati huyu yanatuonyesha kwamba, muda mwingi wa maisha yetu hatufanyi kitu chochote kinachohusu afya zetu isipokuwa tunaelekeza nguvu, ujuzi, maarifa na rasilimali nyingine kwenye mambo tu ya kutafuta pesa peke yake. Fikra za waliowengi ni kwamba bado wanaamini kuwa kitu kinachoitwa “afya” kitajileta chenyewe, ilimradi uwe na pesa, na wengine wasiojua wanaamini katika “Pesa Kwanza na Afya Baadae”.

Kwa sasa hali ya afya kwa waliowengi siyo nzuri, na hii ni kutokana na kutokuwa na malengo na mipango inayohusu afya. Mipango mingi inalenga zaidi kujiendeleza kiuchumi, kielimu, kujenga nyumba nzuri, kuongeza uzalishaji, kununua magari n.k. Ni watu wachache wenye kuwa na malengo na mikakati ya kujenga na kuimalisha afya zao. Mara nyingi, watu wanakumbuka kujali afya zao pale wanapougua au kuanza kusikia maumivu. Wataalam na wadau wengine wa masuala ya afya, wanatwambia kwamba, pale unapoanza kujisikia maumivu ndani ya mwili au kuumwa kabisa, basi ujue kuwa umechelewa kula chakula kama dawa. 

Mara nyingi, imekuwa ni kawaida kuletewa chakula bora pale tunapokuwa tayali tunaumwa na kulazwa hospitalini, ndiyo maana ukitembelea wagonjwa, unapishana na watu wakipeleka machupa makubwa ya jwisi na matunda ya kila aina. Vyakula hivi ambavyo tunaletewa tukiwa wagonjwa, hakuna mtu anayeweza kukuletea tena nyumbani kwako ukiwa mzima, kwasababu, ni matarajio yetu kuwa, ukisharudia hali yako nzuri kiafya, utachukua jukumu la kuendelea kujali afya yako wenyewe. Lakini, cha ajabu, hatufanyi hivyo mpaka tunapoletewa vyakula kwa mara nyingine, pindi tunapougua tena!. Ukweli ni kwamba, jambo la kuimalisha na kulinda afya zetu tumelichukulia la mzaa sana. Kwahiyo, ni muhimu sana tukatambua kuwa mafanikio makubwa tunayotafuta kwasasa yataweza kufikiwa kwa haraka iwapo tutazipa afya zetu kipaumbele namba moja, nje ya hapo maisha bora yatabaki kuwa ndoto ya milele.

Ukitafakari kwa kina sana, utagundua kuwa afya bora ndiyo machimbo ya kudumu ya “Pesa” tuliyonayo. Afya bora ndio utupatia rasilimali “nguvukazi”na pindi nguvu kazi yetu tunapoiwekeza kwa ufanisi hasa katika shughuli za uzalishaji ndipo tunapata bidhaa au huduma ambazo watu wengine utoa na kuleta pesa kwetu, ili kujipatia bidhaa/huduma husika. Pesa ndiyo utuwezesha kupata mahitaji yaliyo mengi kwa muda tunaoutaka na hatimaye kufikia maisha bora ambayo ndiyo ndoto yetu ya muda mrefu.

Kwakuwa, pesa tuipatayo, chimbuko lake ni afya bora, ni muhimu kwa kila shilingi ya pesa tunayoipata, mgao wa kwanza uelekezwe kwenye kuimalisha na kulinda afya. Tunasema suala la matumizi ya pesa kwenye afya, liwe ndio kipaumbele namba moja kwasababu afya ndiyo kisima chetu cha pesa. Unapoamua kutenga pesa kwaajili ya afya yako, maana yake ni kwamba unazifanya pesa zako kuwa rafiki mkubwa wa mwili wako. Pesa zinakuwa rafiki yako pale unapozitumia kujenga, kuimalisha na kulinda afya yako kwa ujumla. Pesa haziwezi kuwa rafiki wa mwili wako, kama hazijatumika kulisha chembe hai za mwili kupitia ulaji wa vyakula na virutubisho muhimu. Nje ya hapo, chembe hai za mwili wako hazina uhusiano na na pesa yako iliyoko mfukoni, benki au kwenye miradi yako ya biashara.

Wito kama unataka mafanikio makubwa anza sasa kuweka malengo ya kupata afya njema na kipato. Ni muhimu vitu hivi viwili viende pamoja kwasababu katika maisha ya Ujasiriamali, vinategemeana sana na vinapoungana ndiyo tunapata furaha ya kweli. Kwahiyo, jitahidi sana kujali afya wakati wote wa safari yako ya kusaka mafanikio ili ukifika maisha ya ndoto yako uwe una afya njema na hapo utafurahia zaidi kuliko anayeumwa kwasababu aliunyima sana mwili wake wakati wa safari ya kusaka mafanikio.

MAAMBUKIZI KUPITIA NJIA YA MKOJO (UTI) YANAATHIRI WANAWAKE WENGI TANZANIA
Wanawake wanapata ugonjwa wa UTI kwa urahisi sana kuliko wanaume kwa sababu  mirija ya mkojoya mwanamke ni mifupi ambayo huruhusu bacteria kuingia kwa urahisi tofauti na ya mwanaume. Katika magonjwa yanayosumbua wanawake wengi na watoto nchini hivi sasa ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo yaani U.T.I (Urinary Tract Infection). Wakati wanawake wengi wanaougua ugonjwa huu wakihangaika kila siku kupata tiba yenye usahihi, wataalamu wa afya wanasema UTI inapojihimarisha mwilini kwa muda mrefu huathiri figo pia.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Afya ya Uzazi kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dk. Cyriel Massawe  anasema, tatizo hili hujitokeza pale mlango wa njia ya haja ndogo unaposhambuliwa na bakteria ambao husambaa na wasipotibiwa mapema, huenea hadi kwenye figo na athari zake ni mbaya.
“Bakteria hawa hupatikana ndani ya sehemu za siri za mwanamke, bakteria hao wakiwa ndani ya uke hawana madhara kabisa, lakini pindi uke unapopata mchubuko bakteria hawa huanza kuathiri kibofu cha mkojo na mtu kuanza kupata madhara,” anasema na kuongeza: Wanawake wanapata UTI kwa urahisi sana kuliko wanaume kwa sababu  mirija ya mkojoya mwanamke ni mifupi ambayo huruhusu bacteria kuingia kwa urahisi tofauti na ya mwanaume.

Vyanzo vya UTI
        i.            Matumizi ya maji  machafu wakati wa kujisafisha au kuoga huweza kuweka bakteria kwa urahisi na mwanamke kupata UTI. 
     ii.        Uchafu wa vyoo umetajwa kuwa sababu nyingine, kwani matumizi ya vyoo ambavyo ni vichafu huweza kusababisha mwanamke kupata UTI kwa sababu ndani ya choo kuna bakteria wengi ambao wanaweza kusababisha UTI.
    iii.           Kufanya ngono mara kwa mara ni tatizo kubwa ambalo ndilo linafanya wanawake wengi kupata UTI siku hizi, kwani wakati wa ngono msuguano huwa mkubwa ambao hufanya bakteria kutoka kupitia majimaji ya ukeni na kuingia katika njia ya mkojo. “Mwanamke ambaye anafanya ngono mara kwa mara yuko kwenye hatari ya kupata UTI kuliko yule ambaye hafanyi ngono mara kwa mara.
    iv.            Matumizi ya nguo za ndani za mitumba bila kufua husababisha kwa urahisi mwanamke kupata UTI,” anasema.
      v.            Matumizi ya vipodozi na sabuni zenye "KEMIKALI" Ambazo zinawaathiri wanawake wengi siku hizi,  kutumia sana kemikali hasa kwenye vipodozi na sabuni ambavyo kemikali hizi kwa kuwa ni sumu huenda hadi kwenye kibofu na kuchubua kibofu na hapo ndipo tatizo hilo huanza.”
    vi.       Tabia tabia ya kubana mkojo kwa muda mrefu, lakini matokeo ya tabia hii ni kupata UTI:

No comments: