Monday, November 30, 2015

Kisa cha Wewe Kuitwa Bahili ni Hiki

“Watu wengine wameitwa wabahili kwasababu wameamua kudhibiti pesa zao zisichukuliwe kiholela na watu wengine”.

Imekuwa ni kawaida kusikia watu wakilalamikia wenzao kuwa ni wabahili. Wengine wanasema eti hawa wanaoitwa wabahili ni wagumu sana kupata pesa yao!; pia inasemekana kwamba watu hawa hawapendi pesa yao itoke kwenda kwa watu wengine ~hawataki kutoa riziki.
Pengine ni vizuri tujiulize ni kwa namna gani mtu anaitwa bahili?

Saturday, November 21, 2015

Sababu ya Wewe Kutopata Mtaji Imebainika

“Ukipata pesa na ukaitumia kabla ya kutenga akiba, basi ujue umelipa watu wengine kwanza na wewe umesahau kujilipa” 
Tajiri mkubwa na mashuhuri duniani, Bwana Warren Buffet aliwahi kusisitiza kuwa, kama unataka kujenga mtaji kutoka kwenye akiba yako binafsi ni sharti ujitahidi kuacha tabia ya “kuweka akiba baada ya kutumia na badala yake utumie kile kinachobaki baada ya kutenga pesa ya akiba”. 

Katika maisha ya umilikaji pesa duniani, kuna makundi ya aina mbili......

Saturday, November 14, 2015

Kupata Mapato Makubwa Kunahitaji Jambo Moja Muhimu

“Hakuna aliyewahi kulipwa pesa nzuri kwa kugundua matatizo, isipokuwa wale wanaotatua matatizo ya watu wengine wengi”
Pesa huwa inatiririka zaidi kuelekea kwa mtu yeyote aliye na suruhisho la matatizo au changamoto mbalimbali zilizoko kwenye jamii.

Kwa kawaida ni kwamba, thamani ya suruhisho lako ni......

Tuesday, November 10, 2015

Ni Marufuku Kuwa Mjasiriamali

"Fahamu Sababu 5 Kwanini Wewe Hutakiwi Kuwa Mjasiriamali"

Mpendwa msomaji wa mtandao huu wa MAARIFASHOP, utakumbuka kuwa ni mara nyingi nimekuwa nikiandika sana juu ya ujasiriamali, na sababu za kufanya hivyo kwa sehemu kubwa ni kwamba ujasiriamali ndiyo njia ya uhakika ya mtu yeyote kuweza kuwa kiongozi wa maisha yake. Lakini...

Saturday, November 7, 2015