Tuesday, May 31, 2016

Mbinu Hizi za Kupata Pesa Zinakufaa



 "Visingizio ndio misumari ya kujenga daraja la kushindwa" ~ Cypridion Mushongi

 

Kupata pesa kunahitaji vitu vingine zaidi ya pesa. Vitu vingine zaidi ya pesa ni pamoja na wewe kufahamu na kujifunza tabia na mbinu mbalimbali wanazotumia wale waliofanikiwa tayari. Kwakusoma makala hii tayari umekwisha anza safari yako ya kutengeneza pesa nyingi na hatimaye kuishi maisha ya ndoto yako.

Ni vizuri safari yako ikaanza kwa kufahamu kwanza mbinu hizi tisa ambazo ni muhimu ukazitumia katika harakati zako za kujenga utajiri kwa sasa na siku za usoni.
 Mbinu hizi ni

Wednesday, May 25, 2016

Hii Ndiyo Hasara ya Kulipa Kwanza Watu Wengine


“Unapopata pesa ukatenga akiba kwanza, tunasema umejilipa kwasababu pesa hiyo imebaki kwako na ndiyo mbegu ya kuzalisha pesa nyingi zaidi” ~ Cypridion Mushongi
 
Watu wengi tunajua kuwa ukishafanya kazi ya mwajiri kinachobakia ni kulipwa mshahara au ujira, nje ya hapo hatuna habari. Ukilipwa na mwingine unafurahi sana. Furaha unayoipata ukiwa umelipwa mshahara, pengine ndiyo inakusukuma kutumia mara moja kipato chako kila unapolipwa. Hali hii ya kufurahia kulipwa pesa na wengine ndiyo imezidi kutuweka utumwani maisha yetu yote.

Kila tunapolipwa pesa, kazi yetu ya kwanza huwa ni

Wednesday, May 18, 2016

Elimu ya Pesa Yaanza Kupatikana


"Mwanzo wa kutajirika ni pale utakapojua mwelekeo wa matumizi ya pesa yako, ama ni zaidi kwa viingiza pesa au ni zaidi kwa vitoa pesa!"  ~ Cypridion Mushongi

Watu wazima tuliowengi sasa hivi tunajua kusoma na kuandika. Tumepitia kwenye njia na hatua nyingi, ikiwa ni pamoja na kutumia gharama kubwa kwaajili ya kutafuta kuelimika na kufuta ujinga tuliokuwa nao. Tunamshukuru Mungu, hicho ni kitu kimoja ambacho shule zetu zinakifanya vizuri. Lakini,...

Wednesday, May 11, 2016

Ukweli Kuhusu Mwekezaji ni Huu


“Usitegemee kipato kutoka kwenye chanzo kimoja peke yake BALI wekeza ili kutengeneza chanzo cha pili” ~ Warren Buffet
 
Bilashaka wewe unayesoma makala hii, umesikia mara nyingi maneno kama “uwekezaji, mwekezaji n.k. Pengine niseme kuwa, kwa nchi kama Tanzania ambayo iliwahi kuongoza na kuendesha siasa zake pamoja na uchumi wake kwa kufuata falsafa na kanuni za mifumo ya ujamaa na hata ukomunisti, neno “uwekezaji na wawekezaji” ni vitu ambavyo ni vigeni na vinachukuliwa kuwa ni kazi ambazo ni maalum kwa wazungu!. Watanzania wengi bado hawaamini kama mtanzania tena ambaye ni