Tuesday, October 27, 2015

Fanya Mambo 5 Leo Kufaidi Nguvu ya Fikra Zako

Fanya Mambo 5 Leo Kufaidi Nguvu ya Fikra Zako


Fikra zetu kutoka ndani ya akiri zetu ndiyo kila kitu. Fikra ndilo dirisha unalotumia kuangalia dunia na mambo yake yote. Ukishakuwa umelitabua hili utakubaliana na mimi kuwa unahitaji kuanza mara moja kujitathimini juu ya mwenendo wako. Unahitaji, kujenga na kuinua heshima yako juu na hii ikiwa ni pamoja na kupanua dirisha lako la fikra ili kuona zaidi fursa za mafanikio. 

Ili kupanua dirisha la fikra, inabidi kutunza  kujiamini na kujikinga dhidi ya athari zitokanazo na changamoto mabalimabali za kimaisha. 

Na hapa unahitaji kufahamu mambo 5 yatakayo kuwezesha kufanya uchunguzi wa undani ya fikra zako na hatimaye kupata msingi imara wa kuweza kuzijenga upya, ili ziwe katika mwelekeo ambao ni chanya. 

Ninatumaini kuwa, ukishakuwa umefahamu nini cha kufanya, basi utaweza kufahamu ni kitu gani unatakiwa kufanya na ni kwanini ni muhimu kwako.
Katika kuchunguza undani wa akiri yako na hatimaye kupanua dirisha lako la fikra zako, unahitaji kufikiria mambo 5 ya msingi:

1.      Jua Kuwa Maisha Yako, Yanatengenezwa na Fikra Unazozipa Kipaumbele Kila Siku.
Ukisoma kitabu cha Bwana James Allen kiitwacho “As a Man Thinketh” anatoa mafundisho ya kwamba, wewe binadamu ndiye unayetengeneza au kuharibu maisha yako mwenyewe kutokana na fikra juu ya fikra ulizonazo akirini mwako. Na pale unaporuhusu mawazo yatokee unakuwa ni muhanga wa maelfu ya mawazo hasi na imani finyu zinakuzunguka kupitia duara lenye taarifa hizo kila muda unaopita.

Unapokuwa mfikiriaji mahili wa mawazo (mtu mwenye kufikiri na kuchagua kile unachofikiria), basi jua kuwa hapo una uwezo wa kujenga maisha ambayo ni chanya na kutembea kila siku kuelekea kwenye ndoto yako ya maisha mazuri.

2.      Jua Kuwa Kubadili Kitu Chochote Nje ya Wewe, Lazima Ubadili Fikra Zako Kwanza.
Kama unataka watu wengine wabadili mtazamo wao wa jinsi wanavyochukulia au kukuona, lazima uanze kujibadili wewe kwanza. Kama unataka kubadili uchumi, jibadili wewe. Kama unataka kubadili hali ya maisha, jibadili wewe mwenyewe. Kama unataka kubadili dunia, jibadili wewe mwenyewe. Hiyo ndiyo kazi ya ndani yako ambayo utengeneza upenyo halisi na kuelekea kwenye mafanikio.

3.      Jua Kuwa Fikra Chanya Hazijengwi kwa Siku Moja.
Mwelekeo wa fikra ulizonazo ziwe chanya au hasi, zinajengwa ndani ya mzunguko wa siku 30. Baada ya siku 30 za kufanya kitu fulani, jua kwamba imekuwa tabia yako. Na maoni yako juu ya mwenendo wa maisha uliyonayo, pia ni matokeo ya tabia ya fikra zako za kila siku. 

Kwahiyo, usifanye kitu hiki siku ya Jumatatu peke yake na kutarajia kuwa millionia siku ya jumanne. Tambua kwamba ukiweka siku 30 za kufikiri mambo chanya fikra zako zitabadilika kwa kiasi kikubwa sana. Na baadae unapanda viwango kwenda hatua nyingine ya juu zaidi na kuendelea…

4.      Jua Kuwa Unatengeneza Maisha Mazuri kwa Kujenga Taswira Nzuri Mwenyewe.
Taswira yako inatengenezwa na picha ya iliyoko kwenye ubongo na ambayo inachezesha fikra zako kwa siku nzima. Ni jinsi gani unavyojiona wewe mwenyewe kufanikiwa au kutofanikiwa. Ndiyo sababu, jambo namba moja hapo juu ni muhimu sana.

5.      Jua Kuwa Kile Unachokiamini Ndicho Kinawezekana
Kama kweli unaamini unaweza kufanya chochote na ukafanyia kazi imani hiyo, basi kwa hakika utaweza kufanikisha ndoto yako. Ni lazima uamini kuwa unaweza kufanya kitu chochote. Unaweza kuimba kwamba “unaaamini unaweza kupaa,” lakini hauamini kwamba unaweza kufanya hivyo na kwahiyo, sheria ya uvutano bado inafanya kazi. 

Na inaweza kuwa kukuhamasisha ukajikuta unapendekeza kuwa unaweza kusogeza mlima kwa kutumia mbegu ya ndogo sana ya zao la ulezi, lakini wote tunajua kuwa hicho ni kitu ambacho hakiwezi kutokea. Lakini unapokuwa umeweka malengo, unaweza kwa dhati ukayatimiza kwa kwenda kuyafanyia kazi, na ikawezekana kuwa hivyo. Hakikisha kuwa unafanya kazi na kutimiza majukumu yako ya kila siku yanayohusu maendeleo yako binafsi.

Jitahidi kuweka fikra chanya na kujua kwamba sehemu yako ya ubongo inayoitwa subconscious itakuongoza wewe kuchukua hatua moja baada ya nyingine hadi kufanikisha hicho ulichokipanga kukifanya kuwa dhahiri. Endapo utakuwa umenielewa nazungumzia nini juu kuchukua hatua dhidi ya ya mambo 5 hapo juu, basi hapana shaka unaweza kuishi ndoto zako. Na hiki ndicho ninachokutakia ukifanye.

Mpendwa msomaji, endelea kuitumia vizuri MAARIFASHOP ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuwezesha kupata mafanikio. Ili kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza neno TUMA MAKALA MAARIFASHOP kisha sajiri barua pepe yako. Na kama unapenda kupata mafunzo ya kila siku kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO

No comments: