Nikiwa mmojawapo wa washiriki wa kikao cha kamati ya mradi wa kilimo siku ya tarehe 13/07/2017, mwenyekiti wa kamati alifungua kikao na kukumbusha wajumbe kuwa mojawapo ya majukumu ya kamati ni pamoja na kupanga namna bora ya uendeshaji wa shughuli za mradi.
Katika kusisitiza hilo alisema “kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa”. Maneno haya yalinigusa sana na yalinifanya kutafakari zaidi juu ya maana ya maneno haya katika maisha yetu ya kila siku.
Katika maisha kuna vitu ambavyo vipo na havitegemei uwepo wako. Vitu ambavyo havitegemei uwepo wako ni