∞∞∞ "Ni bora kuishi na mtu aliyeshindwa kuliko mtu mwenye Mashaka ~ Cypridion Mushongi" ∞∞∞
Biashara ni mradi au mfumo unaotengenezwa na mjasiriamali kwa lengo la kuzalisha bidhaa au huduma inayokidhi mahitaji ya wanajamii (wateja) mbalimbali duniani.
Wakati wote, biashara inapoendelea kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, hapo tunasema kuwa “Biashara yako ni hai na inaishi”. Tunasema biashara “imekufa” endapo..
itashindwa kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake ambayo ni kushindwa kuzalisha bidhaa au huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja wake.
Yako mambo mengi yanayoweza kuua biashara yako na katika ya hayo kuna yale ambayo ndiyo hasa chanzo cha kifo. Ukiuliza kinachoua biashara, mara nyingi utaambiwa vitu vile vilivyozoeleka, lakini ambavyo siyo chanzo kikuu.
Vitu utakavyoambiwa ni kama: “hakuna mzunguko wa pesa, mtaji mdogo n.k. Lakini ukweli ni kwamba kuna vitu ambavyo havitiliwi maanani lakini kimsingi ndivyo huwa ni kisababishi kikuu kama hivi hapa:
1. Kuwa mtu mwenye mashaka: Mara nyingi “mashaka” ni jambo linaloua biashara nyingi.
Mjasiriamali mwenye mashaka na biashara yake, siku zote anakuwa na tabia ya kutoipa kipaumbele namba moja katika kuwekeza muda, fedha, vifaa, teknolojia n.k. maana yake, mjasiriamali unakaa na mashaka muda wote.
Kuna usemi unasema hivi: "Ni bora kuishi na mtu aliyeshindwa kuliko mtu mwenye Mashaka”.
Inashangaza kuona mjasiriamali unajipa muda mwingi wa kutilia mashaka biashara uliyoanzisha, kuliko muda wa kutafuta ubunifu, teknolojia, fedha kwaajili ya kukuza biashara yako.
2. Kukatishwa Tamaa: Daima kukatishwa tamaa, hufanywa na watu wanaokuzunguka au watu wako wa karibu.
Ni hivi! Unapoona rafiki yako anakwambia kuwa biashara fulani huiwezi ni ngumu, maana yake anakwambia kuwa ugumu huo, uko kwake yeye. Lakini anaongea kwa sauti kana kwamba huo ugumu ni kwako wewe.
Unapoona mtu anaongelea kuhusu ugumu wa kufanya biashara fulani, tambua kuwa mtu huyo anajaribu kukuuzia ugumu alionao yeye juu ya biashara hiyo unayotaka kuifanya.
Kama ukimkubalia kwasababu tu! ni ndugu au rafiki, basi ujue kuwa umeamua KUNUNUA ugumu na yeye AMEUZA kwako. Kwahiyo, mwisho wake utakachokipata ni kushindwa!
Kukatishwa tamaa mara nyingi hufanywa na watu ambao kimsingi tunawaita “watafutaji” wa pesa. Kama wewe ni mjasiriamali yaani "mtengenezaji" pesa, tambua kuwa watakaokuja kukukatisha tamaa ni watafutaji ambao siyo wenzako.
Mtafutaji hawezi kuwa rafiki wa mjasiriamali (mtengenezaji), kwasababu mnatumia mfumo na mtindo tofauti wa maisha.
Maswali ya kujiuliza ni je, mtafutaji ni nani? Na je, mtengenezaji ni nani? Nitawatofautishaje ili nijue nani wa kumsikiliza? Majibu ya maswali haya utayapata kwenye makala zitakazochapishwa siku za usoni hapa MAARIFASHOP.
3. Kuwa na Hofu: Mara nyingi, hofu huwa ni jambo LA kufikirika au hisia tu! siyo uhalisia wa mambo.
Hofu hukuzuia kuanza kufanya biashara na siku zote, mtu mwenye hofu anakuwa na tabia ya kusitasita katika maamuzi ya kuchukua hatua.
4. Fikra Hasi: Kuwepo kwa fikra hasi kunatokana na ukweli wa kanuni ya sayansi inayosema kwamba "Chanya Huvuta Hasi".
Unapoanzisha bisahara, kwako wewe hilo ni jambo "Chanya".
Ndiyo maana, biashara ikianza tu! Unaanza kukumbana na mambo "Hasi" kutokana na ukweli kwamba, biashara yako (Chanya) imeanza kuvuta "Hasi".
Ukianza kukumbana na hali hiyo usilalamike badala yake jikite katika kutafuta namna ya kuondoa au kupunguza athali zake.
Unapokumbwa na jambo lolote ambalo ni "Hasi" libadilishe kwa kuweka mambo matano (5) ambayo ni "Chanya".
Umahiri wako katika kujenga na kulinda biashara yako isife, ndio unakujengea “UJASIRI WA KUTAFUTA MALI”. Ukifikia hatua hii, jamii inakupa hadhi ya kuitwa MJASIRIAMALI.
Kwa wajasiriamali wa zamani na wale wapya, endelea kupata MAARIFA yatakayokuwezesha kupata mafanikio.
Ili kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza neno MAKALA MPYA kisha sajiri e-mail yako.
Kwa wale wanaopenda kupata mafunzo kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO.
KARIBU WOTE KATIKA KUSAKA MAARIFA!
1 comment:
PESA AU UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI,, NDAGU NA PETE YA BAHATI,,
======= KUTANA NA MGANGA BINGWA WA TIBA ZA ASILI ,,BINGWA WA TIBA ZA MAPENZI ,,BIASHARA NA KUKUPA UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI NA NDAGU,, SI MWENGINE NI DR.Mdiro
MAWASILIANO
WHATSAPP +255742162843
KWA WALIO NJE YA NCHI TUMIENI WHAT'S UP KWA MAWASILIANO
Malipo ni baada ya mafanikio
====Natibu magonjwa sugu kisukali presha kifafa nguvu za kiume uzazi chango ngiri busha ganzi miguu,,tumbo gesi,,maumivu ya mwili,,ndoto mbaya,,na kutafasri maana ya ndoto unazo ota ,, nk
===== Nasafisha nyota,,kutoa mikosi,,nuksi,,kutoa majini mabaya,,kutoa chuma ulete kwenye biashara,, kupandishwa nyota,, kupandishwa cheo,, kupata kazi,, kushinda kesi,,kulipa kisasi kwa ulicho fanyiwa nao wajisikie vibaya Kama wewe ilivyo jisikia,,nk
===== Kumrudisha mpenzi mchumba mume mke uliye tengana nae ,,au kakutelekeza,, kumshika mme wako au mpenzi wa mtu awe anakusaidia na kukutimizia mahitaji Kama NI mpenzi wako,, au Kama anakutaka awe anakupa pesa bila kumuomba ,,
===== Kumrudisha mke mme kwenye himaya yako tena kama mmeachana na unahitaji muwe pamoja au muishi wote Kama zamani,,au Kama humuitaji yeye unataka pesa zake tu pia atakusaidia hata bila kumpa pezi lako,,
=====Kumilikishwa Mali au utajiri mkubwa wa majini,, kupata utajiri mkubwa wa ndagu,,kupata utajiri mkubwa wa freemason,, kukupa utajiri mkubwa kuliko wengine utajiri wa Pete ya bahati ambayo itakuvutia mali pesa na itakupa mvuto mkubwa wa kupendwa na watu,,
===== Kukupa chuma ulete,,kukupandisha nyota ya uganga,, kukupa karama ya kumiliki uchawi,, kukupa nyota ya kushinda bahati nasibu au kamali,, kukupa kinga ya kiwaona wabaya ,, kuona matatizo yako,, kukupa mvuto mkubwa wa kuolewa au kuoa Kama unamchumba au huna kabisa yaani ajitokezee mwenyewe aseme anataka kukuoa au umuowe,,
===== NJOO NIKUHUDUMIE,, PIA NATIBU HATA UKIWA MBALI NAMI UWE MKOANI AU NCHI NYINGINE HUDUMA UTAIPATA KWA HARAKA NA UTAFANIKIWA KWA MDA MFUPI TU,,
====KWA UTAJIRI MKUBWA WA MAJINI
====KWA UTAJIRI MKUBWA
Post a Comment