Tuesday, February 10, 2015

UNAPOAMUA KUANDIKA HISTORIA YA MAISHA YAKO USIKUBALI MTU MWINGINE AKUSHIKIE KALAMU



Kwakuwa maisha ni safari ambayo unasafiri muda mrefu kabla ya kufika unakokwenda au kufikia maisha ya ndoto yako. Wakati ukiendelea na safari yako ya maisha, usikubali kushawishiwa na mtu yeyote wala kundi lolote lile kwani wao ni vigumu sana kufahamu unakotaka kwenda. Usijaribu hata siku moja kuchagua njia au cha kufanya kutokana na matakwa ya watu wengine.
 Mtu kikundi Fulani kufanya jambo Fulani na wakashindwa haimanishi kwamba na wewe utashindwa kumbuka wewe unajifanana wewe peke yako, hakikisha haugopi kupigwa mishale kutoka kila kona ambayo ni kejeli, matusi, kubaguliwa, kutengwa, kusemwa vibaya n.k. Jitahidi kuwa na uamzi pamoja na uchaguzi binafsi kama njia mojawapo ya kufikia mafanikio unayoyahitaji. Kwahiyo nilazima ujifunze kusema hapana kwa baadhi ya vitu, hata kama vinafanywa na watu wengi. Jambo la kuwa na uchaguzi na uhamzi binafsi ni muhimu sana kwani usipojifunza kufanya hivyo, basi wewe kila wakati utakuwa mfanyakazi au mtumwa wa kutumikia uchaguzi na uhamzi wa watu wengine. Ili uweze kuwa na uchaguzi sahii wa jambo la kufanya ili kupata mafanikio na maisha mazuri ni lazima kujifunza kutofautisha kilicho muhimu na kisicho na umuhimu. Watu waliowengi wanafanya vitu vingi, hata kama vingine siyo vya muhimu ilimradi tu watu wengine kama marafiki ndugu n.k wanafanya basin aye atafanya.
Matokeo ya kufanya kila kitu eti kwa sababu wengi wanafanya, ni kujikuta muda wako mwingi unautumia Katika vitu au shughuli ambazo zinaleta mafankio kidogo sana. Mwandishi “Richard Koch” Katika kitabu chake cha “Living the 80/20 Way: Work Less, Succeed More, Enjoy More”anasema kwamba ili uweze kupata mafanikio makubwa maishani ni lazima utumie Asilimia 20% ya muda kupata mafanikio ya Asilimia 80%; Kwahiyo, mwandishi huyu anatufundisha kuwa iwapo utakuwa mtu wa kufanya kila kitu ili mradi wanafanya marafiki zako, basi ujue wewe utakuwa unatumia Asilimia 80% ya muda wako ili kupata mafanikio ya Asilimia 20% tu! Kwa maana nyingine wewe utakuwa mtu unayehangaika kila siku mpaka unakufa.
Ikumbukwe kuwa Katika maisha unapoamua kuchagua kufanya kitu kimoja kati ya vingi ulivyonavyo, siyo kwamba hivyo vingine huvihitaji bali unachagua kilicho bora zaidi. Kufanya maamuzi ni mwanzo tu wa vitu kutokea na inampelekea mtu kupata nguvu halisi ambayo itampeleka mahali ambapo ni pazuri na hata unakuta mwanzoni ukupafikiri wakati ulipoamua kufanya mabadiliko hayo.
Katika kuandika historia ya maisha yako, uwezi kumfurahisha kila mtu, hivyo huwezi kukamilisha kila kazi unayo paswa kuifanya. Kwahiyo katka kila kazi au majukumu ni vizuri ukaweka malengo na utendaji wako ukawa unaongozwa na malengo uliyojiwekea wewe mwenyewe,  hivyo kipimo cha kufanikiwa au kutokufanikiwa kwako kitakuwa ni kwako kuweza kujipima kwa kutimiza au kushindwa kutimiza malengo yako na si kusikiliza watu wanasema nini kuhusu kufanikiwa au kutofanikiwa kwako.

Mpendwa msomaji, endelea kuitumia vizuri MAARIFASHOP ili kujifunza mambo mbalimbali yatakayokuwezesha kupata mafanikio. Ili kupata makala mpya kila zinapochapishwa, bonyeza neno TUMA MAKALA MAARIFASHOP kisha sajiri barua pepe yako. Na kama unapenda kupata mafunzo ya kila siku kwa njia ya whatsap bonyeza neno MAFUNZO

KARIBU TUCHUKUE HATUA PAMOJA!

No comments: