Monday, August 28, 2017

Fursa Nyingi Tuko Maskini Kwanini?


Mapema leo 28/08/2017, nilikuwa naangalia na kusikiliza video juu ya kongamano la wadau wa zao la mpunga, lililofanyika kuanzia tarehe 14-18 mwezi septemba 2015. Mkutano huo ulihusisha zaidi wanasayansi na wataalam wa kilimo cha mpunga. 

Katika mkutano huo, mmoja wa washiriki ambaye ni Profesa Nuhu Hatibu aliwasilisha mada yake iliyojulikana kama “Biashara ya kikanda kwa mazao ya chakula kama nyenzo ya kuufanya utafiti utumike katika kutengeneza utajiri” au kwa lugha ya Kingereza; “Regional Trade in Food Staples as an Instrument for Getting Research into use for Wealth Creation”. Katika video hiyo Profesa Nuhu Hatibu, alitoa nasaa za maana sana na akaeleza

Monday, August 14, 2017

Unajua Kwanini Kwanini Yako ni Muhimu?


"Kwanini yako" ndiye mlizi wako dhidi ya changamoto na wakatisha tamaa" ~ Cypridion Mushongi
Kwa mtazamo wa kimafanikio, kuweza kuuishi ukweli ni muhimu katika kufikia malengo yako hasa, uhuru wa kipatao/fedha. Jaribu kufikiria ulipokuwa bado mdogo, wakubwa zako walikuuliza unataka nini ukikua, pengine ulisema unataka kuwa mwanasayansi mashuhuri, mpishi, mwimbaji au daktari wa mifugo n.k. Na unaweza kukumbuka walionekanaje ulipowapa majibu hayo? Yawezekana walikukatisha tamaa kwamba haiwezekani au walikutia moyo kwa kukwambia kuwa unaweza ukawa mtu yeyote unayetaka kuwa, ilimradi

Monday, August 7, 2017

Sababu za Wateja Kuwa Zaidi ya Bosi ni Hizi Hapa


Katika maisha yetu ya kila siku, matendo yetu sikuzote yanadhihirisha na kuthibitisha kile tunachofikiri na kuwaza. Hii ndiyo kusema kwamba, kitu cha kwanza na muhimu kuwa na maisha bora yanayoambatana na uhuru wa kifedha ni jinsi tunavyofikiri na kutenda. Watu wengi wanafikiri mpaka watakapokuwa na mali nyingi ndipo watajiita au kujiona matajiri. Suala la kuwaza wengi wetu hatulipi kipaumbele, kiasi kwamba wengine wanadhani kukaa na kufikiri ni

Monday, July 31, 2017

Muuzaji na Mnunuzi Nani ni Mfanyabiashara?


Katika maisha yetu ya kila siku hapa duniani, kuna watu wanaofikiri na kuamini “sisi siyo wafanyabiashara wao ni wafanyabiashara”. Wengi wanaamini kuna kundi fulani la wafanyabiashara. Kutokana na mtazamo huu juu ya biashara, wengi wanajiaminisha kuwa wanaweza kuishi maisha mazuri bila kuwa wafanyabiashara. 

Watu wengi wanadahani mfanyabiashara ni

Monday, July 24, 2017

Hatari ya Kushindwa Kupanga ni Kama Hii



Nikiwa mmojawapo wa washiriki wa kikao cha kamati ya mradi wa kilimo siku ya tarehe 13/07/2017, mwenyekiti wa kamati alifungua kikao na kukumbusha wajumbe kuwa mojawapo ya majukumu ya kamati ni pamoja na kupanga namna bora ya uendeshaji wa shughuli za mradi. 

Katika kusisitiza hilo alisema “kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa”. Maneno haya yalinigusa sana na yalinifanya kutafakari zaidi juu ya maana ya maneno haya katika maisha yetu ya kila siku.

Katika maisha kuna vitu ambavyo vipo na havitegemei uwepo wako. Vitu ambavyo havitegemei uwepo wako ni