Mapema leo 28/08/2017, nilikuwa naangalia na kusikiliza video juu ya kongamano la wadau wa zao la mpunga, lililofanyika kuanzia tarehe 14-18 mwezi septemba 2015. Mkutano huo ulihusisha zaidi wanasayansi na wataalam wa kilimo cha mpunga.
Katika mkutano huo, mmoja wa washiriki ambaye ni Profesa Nuhu Hatibu aliwasilisha mada yake iliyojulikana kama “Biashara ya kikanda kwa mazao ya chakula kama nyenzo ya kuufanya utafiti utumike katika kutengeneza utajiri” au kwa lugha ya Kingereza; “Regional Trade in Food Staples as an Instrument for Getting Research into use for Wealth Creation”. Katika video hiyo Profesa Nuhu Hatibu, alitoa nasaa za maana sana na akaeleza



